
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, matukio mapya ya usalama yanavuruga mwitikio wa mlipuko wa virusi vya Ebola. Siku ya Jumatano, Julai 15, huko Nyankunde, katika sehemu ya mashariki ya nchi, kilomita 45 kusini magharibi mwa Bunia katika mkoa wa Ituri, wanamgambo walirushiana risasi karibu na kituo cha matibabu ya Ebola. Katika tukio lingine kama hilo, wanaume wenye hasira walirusha mawe katika majengo ya kituo hicho.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Hali halisi ya shambulio la Kituo cha Matibabu cha Ebola cha Nyankunde (ETC) bado haijulikani wazi. Inaonekana kulikuwa na matukio mawili tofauti. Kulingana na maelezo kadhaa, wanamgambo wa eneo hilo walirushiana risasi; mmoja wa viongozi wa wanamgambo hao aliuawa.
Matukio yote mawili yalisababisha hofu. Siku ya Alhamisi, wafanyakazi waliohusika na mwitikio wa janga hilo waliondoka katika eneo hilo kwa sababu za kiusalama.
Wakati huo huo, familia ya mwanamke mjamzito aliyefariki katika kituo hicho cha matibabu ilijaribu kuchukua mwili wake na, kwa hasira, ikarusha mawe katika kituo cha matibabu.
Matukio yote mawili yalisababisha hofu. Katika hali hiyo, wagonjwa wanne wa Ebola walitoroka. Kulingana na afisa katika kituo cha matibabu, wagonjwa wote wanne wa Ebola wamerudi katika kituo cha Nyankunde. Hata hivyo, mgonjwa mmoja anayeshukiwa kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo alitoroka.
Wafanyakazi wa afya wameamua kuondoka katika eneo hilo
Siku ya Alhamisi asubuhi, wafanyakazi wa afya kutoka Shirika la afya Duniani (WHO), Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), na shirika lisilo la kisetrikali la Samaritans Purse waliamua kuondoka Nyankunde kwenda Bunia.
Dkt. Yap Boum, mkuu wa kitengo cha majibu ya dharura katika Africa CDC, ana wasiwasi kuhusu kuondoka kwa timu za majibu, watu wapatao kumi na tano. Mradi tu hali ya usalama si nzuri, anasema, mwitikio wa janga hili una hatari ya kuathiriwa.
“Hii ina maana kwamba eneo hili la afya linazidi kuwa si salama, na eneo lisilo salama la afya linamaanisha kwamba wataalamu hawawezi kulifikia […] Hii inaweza kuathiri shughuli mbalimbali zilizopangwa katika maeneo ya afya ambapo kunaweza kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa walioambukizwa virusi vya Ebola,” anabainisha.