
Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, wamefunga kesi dhidi ya Abdallah Banda, ambayo ilianza mapema miaka ya 2010. Mahakama ilipokea malalamiko ya uhalifu uliofanywa Darfur kutoka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mwendesha mashtaka almshtaki rais wa zamani Omar al-Bashir na kisha waasi kadhaa waliokandamizwa na udikteta wa kijeshi wa Kiislamu. Abdallah Banda, mmoja wa waasi wa zamani wa Darfur, sasa ni mmoja wa makamanda katika jeshi la serikali ya Sudan. Kwa hivyo hatafikishwa Hague. Uamuzi huu ulichukuliwa kwa ombi la ofisi ya mwendesha mashtaka.