Mkuu wa Jeshi la Uganda (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, yuko Kigali kwa ziara rasmi ya kikazi na anatarajia kukutana na rais wa Rwanda Paul Kagame.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Wakati wa ziara yake, Jenerali Kainerugaba atakutana na maafisa wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF) na pia atakutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame.

Majadiliano yanatarajiwa kuzingatia kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na nyanja zingine zenye maslahi kwa pande zote.

Ziara hii inaashiria ziara ya hivi karibuni ya ngazi ya juu ya Jenerali Kainerugaba katika mji mkuu wa Rwanda, ikiangazia kuendelea kuimarika kwa uhusiano wa pande mbili kati ya nchi hizo mbili jirani.

Alipowasili, Jenerali Kainerugaba alilakiwa na mwenzake wa Rwanda, Mkuu wa Jeshi, Jenerali Mubarakh Muganga, mbele ya Kamanda wa Kikosi cha walinzi wa Jamhuri, Meja Jenerali Willy Rwagasana, na afisa wa jeshi la Uganda katika ubalozi wa nchi hiyo nchini Rwanda, Kanali Ezekiel Matsiko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *