SERIKALI imetangaza mpango kabambe wa kuboresha miundombinu ya usafirishaji kwa njia ya barabara wenye lengo la kurahisisha usafiri, kuongeza ufanisi na kukuza Pato la Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam , Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amesema mpango huo unaojulikana kwa jina la Expressways Master Plan sasa umeanza kutekelezwa na wataalamu wazalendo wa Tanzania kwa kushirikiana na wenzao kutoka Korea Kusini.
Waziri Ulega amesema kwa sasa wataalamu wa pande zote wanakutana katika mafunzo maalumu ambayo yatatengeneza dira ya nini kitaenda kutokea kupitia mkakati huo kabambe.
(Feed generated with FetchRSS)