Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM na Mlezi wa CCM Mkoa wa Dodoma, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewaasa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba wanatimiza wajibu wa msingi na wa kudumu wa kuhakikisha CCM inakuwa chama cha Watanzania na kimbilio lao.
Makamu wa Rais, amesema hayo wakati akiongoza Maadhimisho ya Miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi, yaliyofanyika Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, leo tarehe 05 Februari 2026. Amesema wakati CCM ikitimiza miaka 49 bado Watanzania wana imani na Chama hicho, imani iliyodhihirishwa kwa kuchaguliwa kuongoza Nchi.
(Feed generated with FetchRSS)