Los Angeles, Marekani. Kwa takribani miongo miwili, LeBron James amekuwa akichaguliwa kuwamchezaji wa All-Star.

Msimu huu, haikuwa hivyo. Na kwa James, ambaye lengo lake kubwa lilikuwa kurejea akiwa mzima vya kutosha kucheza michezo halisi, hilo halikuwa kipaumbele.

“Kwa kweli sikulifikiria,” James alisema Jumapili baada ya kuchaguliwa kama mchezaji wa akiba na makocha wa Ukanda wa Magharibi kwa mara ya 22 mfululizo, akiweka rekodi katika NBA.

Hiyo ni kwa sababu James, mwenye umri wa miaka 41, hakucheza hadi mchezo wa 15 wa Lakers msimu huu baada ya kuwa nje kutokana na tatizo la sciatica. Hakukosa tu karibu mwezi mzima wa msimu wa kawaida, bali pia maandalizi ya kipindi cha mapumziko (offseason) aliyoyafanya alikuwa kinara wa muda wote wa NBA kwa alama na kuwa mchezaji wa kwanza katika historia kucheza misimu 23.

“Haikuwa lengo langu kuanza msimu, nikose michezo 14 ya mwanzo halafu niseme, ‘Sawa, ninaweza kuwa All-Star,’” James alisema baada ya kufunga pointi 22 katika kipigo cha Lakers 112-110 dhidi ya Knicks, katika mchezo wake wa 32 wa taaluma kwenye Madison Square Garden.

“Nilichotaka tu ni kurejea kucheza kwa kiwango cha juu nilichojua nina uwezo nacho baada ya kuondoa ya kukosa preseason, kambi ya mazoezi, na mazoezi ya majira ya joto, ambayo sijawahi kuyakosa katika maisha yangu yote ya uchezaji. Kwa hiyo sikufikiria kabisa kuhusu Mchezo wa

All-Star.”

James ameongeza kasi tangu siku yake ya kuzaliwa Desemba 30 na kujiunga na Kareem Abdul-Jabbar, nguli wa Hall of Fame aliyempita kuwa kinara wa alama za muda wote, kama wachezaji pekee waliopata chaguo zaidi ya moja la All-Star baada ya umri wa miaka 40.

Kuchaguliwa kwa James kumeibua mjadala fulani jambo ambalo halikutokea mara nyingi katika mfululizo wake ulioanza mwaka 2005 hasa baada ya wachezaji kama Kawhi Leonard na James Harden wa Clippers, pamoja na Alperen Sengun wa Houston, kutochaguliwa.

“Bila shaka anastahili,” alisema mwenzake Luka Doncic, ambaye alichaguliwa kuanza kama mchezaji wa kwanza. “Bado anacheza katika kiwango cha juu akiwa na umri huo. Inashangaza kushiriki uwanja naye.”

James, aliyekosa mchezo wa mwaka jana kutokana na majeraha, pia ni kinara wa muda wote kwa pointi na dakika katika Mchezo wa All-Star. Sasa anaweza kuongeza takwimu hizo katika mchezo wa Februari 15 utakaochezwa nyumbani kwa Los Angeles Clippers.

“Makocha walipiga kura, sivyo? Kwa hiyo nawapa heshima kubwa makocha kwa kuona namna ninavyocheza bado katika hatua hii ya baadaye ya taaluma yangu,” James alisema. “Na kuweza kuwa All-Star kuna maana kubwa kwa familia yangu, kwa watu waliokuwa wakifuatilia taaluma yangu, wafuasi wangu wa LeBron. Wamefuatilia safari yangu, na daima ni jambo la kuthawabisha, kwa unyenyekevu, kupewa tuzo kwa kile ulichowekeza juhudi zako.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *