
Siku kumi baada ya makabiliano makali kati ya jeshi la shirikisho la Ethiopia na Kikosi cha Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF), pande hizo mbili zinashutumiana kwa kujiandaa kwa vita vipya katika eneo hilo. Kutokana na kuibuka tena kwa mvutano, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa anatoa wito kwa pande hasimu kuchukua hatua za haraka kuelekea kupungua kwa mvutano.
Imechapishwa:
Dakika 3 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Tahadhari ya vita vipya inaijia tena Tigray. Hakika, tangu mgogoro kati ya Kikosi cha Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) na jeshi la shirikisho la Ethiopia kati ya Novemba 2020 na Novemba 2022, mvutano haujawahi kuwa mkubwa sana katika eneo hilo. Wasiwasi huo ni mkubwa sana kiasi kwamba Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, alitoa wito siku ya Jumanne, Februari 10 kwa pande hasimu kuchukua hatua za haraka kuelekea kupunguza mzozo haraka iwezekanavyo.
Ikumbukwe kwamba tangu siku iliyopita, pande hizo mbili zimekuwa zikishutumiana kwa kujiandaa kwa vita vipya huko Tigray, ambapo TPLF inataka kurejesha maeneo yenye mgogoro kwenye mpaka na eneo jirani la Amhara, ambapo zaidi ya watu milioni waliokimbia makazi yao bado hawajaweza kurudi. “Baada ya kuanzishwa kwa utawala wa mpito [ulioundwa chini ya Mkataba wa Pretoria uliokomesha vita mnamo mwezi Novemba 2022], serikali ya shirikisho ilishirikiana na baadhi ya watu na maafisa wa eneo hilo ili kuivuruga usalama katika eneo la Tigray.” “Ilitaka kupanga makundi yenye silaha katika maeneo ya Afar, Tselemt, na Agaw, na pia katika Tigray Magharibi,” amesema Amanuel Assefa, Naibu wa kiongozi wa TPLF, katika mahojiano na mwandishi wetu nchini Ethiopia, Marlène Panara. “Na leo, tunaiona ikipeleka wanajeshi kwa wingi kutoka maeneo tofauti ya nchi hadi mipakani mwa Tigray,” amebainisha, akiongeza kwamba anapendelea njia za amani na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kupatanisha.
“Wapumbavu wakubwa”
Serikali ya shirikisho, kwa upande wake, inaishutumu TPLF kwa kuchochea uhasama na kujaribu kutwaa tena maeneo ambayo inadai, kinyume na makubaliano ya Pretoria. “Natumai kwamba wachochezi wa vita ambao ni viongozi wa kisiasa na kijeshi wa TPLF watajirudi na kutambua upumbavu wa matendo yao.” “Natumai wataendelea kufanya kazi kwa karibu na serikali ya shirikisho, na hata kuiwajibisha ikiwa itachelewesha utekelezaji wa makubaliano ya Pretoria,” anasema Getachew Reda, msemaji wa zamani wa TPLF ambaye sasa ni mshauri Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed kuhusu masuala ya Afrika Mashariki. “Lakini kujaribu kuvunja kila mkwamo au kizuizi kwa kutumia silaha si kwa maslahi ya watu wa Tigray. Watu wa Tigray wamebaini wazi kwamba wimbi jipya la migogoro sio kwa maslahi yao,” anaongeza, kabla ya kuishutumu TPLF kwa kushirikiana na Eritrea, ambayo wanajeshi wake bado wapo katika maeneo kadhaa ya mpaka wa eneo la Tigray. Ingawa makubaliano ya amani yaliyosainiwa Pretoria yalibainisha kujiondoa kwao,nakali haijatekelezwa…
“Eritrea inatoa risasi kwa TPLF.” Waeritrea wanataka kuhakikisha mgogoro huo unaelekea kusini iwezekanavyo kwa sababu hawataki mapigano na serikali ya shirikisho kwenye mipaka yao. “Wanachama wa TPLF ni ‘wapumbavu wakubwa,'” anasema Getachew Reda, ambaye anaongeza kuwa “maagizo yaliyotolewa kwa TPLF yalikuwa kujaribu kuunda muungano na waasi wa Fano [wanamgambo wa kitaifa katika eneo la Amhara ambao walichukua silaha dhidi ya serikali ya shirikisho mnamo 2023] huku serikali ya Eritrea ikishughulikia vifaa na usafirishaji. Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la shughuli, ikiwa ni pamoja na kuwasilisha malori kadhaa yaliyobeba risasi na vifaa vingine kwa Tigray.” “TPLF haina muungano na Asmara,” anapinga Amanuel Assefa, kabla ya kufafanua kwamba ikiwa jeshi la shirikisho litatangaza vita dhidi ya Tigray, “tutakuwa na haki ya kuunda muungano wowote kwa sababu itakuwa kujilinda.”
Mapigano makali
Je, kuongezeka huku kwa mvutano kati ya pande hizo mbili kunamaanisha kwamba makubaliano ya amani ya Pretoria yanatishiwa? Ingawa Amanuel Assefa anasisitiza kwamba TPLF imejaribu kushiriki katika mazungumzo na serikali, mapigano yalizuka kati ya pande hizo mbili mwishoni mwa mwezi Januari. Hasa vurugu, zilisababisha vifo vya wanajeshi 1,200 hadi 1,300, kulingana na Addis Ababa, ambayo ndege zake zisizo na rubani zililenga malori ya mizigo siku mbili baadaye.