• Richmond Mensah alisafiri kwenda Uingereza (UK) miaka michache iliyopita kutafuta maisha bora ili kuhudumia familia yake changa
  • Hakujua kwamba jioni moja, alipokwenda kupumzika kidogo kabla ya kuripoti kazini, ingekuwa mara ya mwisho kupumua
  • Watumiaji wa mitandao ya kijamii walivunjika moyo, hasa baada ya taarifa kufichua kuwa muuguzi huyo ameacha mke na watoto wadogo waliomtegemea

Familia changa inakabiliana na uhalisia mchungu wa kumpoteza mpendwa wao, ambaye kwa bahati mbaya alifariki akiwa akifanya kazi ughaibuni.

Richmond Mensah alifariki nchini Uingereza.
Richmond Mensah alikuwa nesi. Picha: Fajira.
Source: Facebook

Richmond Mensah, muuguzi aliyekuwa akifanya kazi nchini Uingereza (UK), alifariki alipokuwa amelala kabla ya kuanza zamu yake.

Alikuwa amepangiwa kufanya zamu ya usiku na akaamua kupumzika kwa muda mfupi ili aamke akiwa amepumzika na tayari kwa kazi.

Kwa masikitiko, alipofumba macho yake ilikuwa mara ya mwisho, kwani alifariki kwa amani akiwa usingizini.

Maneno ya mwisho ya Richmond Mensah kwa mkewe

Mkewe, Maybel, alizungumza kwa hisia kali alipokuwa akijaribu kukubali habari hiyo ya kusikitisha na kusimulia dakika za mwisho za mumewe.

Pia soma

Joseph Mureithi: Shahidi aeleza jinsi jamaa alivyofariki dunia baada ya kutupwa nje ya Super Metro

“Alisema ataweka simu yake kwenye chaji. Nilipoingia mara ya kwanza, alikuwa amelala. Baadaye, kengele yake ililia, lakini hakuwa akijibu. Hapo ndipo nilipopiga 999,” alisema.

Mwenye umri wa miaka 33 alilala saa 10:30 jioni na kuweka kengele saa 11:45 jioni, bila kujua kuwa hiyo ingekuwa siku yake ya mwisho kuwa hai.

Baada ya Maybel kupiga 999, wahudumu wa afya walifika haraka na kuanza jitihada za kumrejesha katika hali ya kawaida kabla ya kumkimbiza hospitalini.

Richmond Mensah alihamia lini Uingereza?

Licha ya jitihada za kumwokoa, alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini. Chanzo cha kifo hakijathibitishwa bado.

Mensah, aliyeacha mke na watoto watatu wadogo, alihamia Uingereza mwaka 2023 kutoka Ghana kutafuta fursa bora.

Alibahatika kupata kazi nzuri, iliyomwezesha kuihudumia familia yake huku pia akiwahudumia wagonjwa kupitia taaluma yake.

Alitumia siku zake za mwisho akiwahudumia wagonjwa kwa huruma, pengo ambalo litahisiwa sana na kuwa gumu kulijaza.

Watu mitandaoni wamuomboleza Richmond Mensah

Watumiaji wa mitandao ya kijamii walionyesha huzuni yao kwa habari hiyo, hasa kwa watoto wadogo watakaokua bila baba yao.

Skosana Shikale: “Saa inapogonga, ni wakati wako, iwe uko Namibia, Marekani au Uingereza. Haijalishi una afya njema kiasi gani au una msongo mdogo kiasi gani, lazima tuelewe kwamba sote tutaondoka duniani, ingawa kwa njia tofauti. Mungu aliita jina lake, naye akaitikia. Pumzika kwa amani, ndugu.”

Pia soma

Mama ya watoto 2 auawa na gari la polisi, familia yazungumza kihisia

Arlene Rowe: “Pole kwa msiba wako. Rambirambi kwa familia na marafiki. Apumzike kwa amani ya milele. Sidhani kama mtu yeyote anapaswa kufanya kazi zaidi ya saa 48 kwa wiki. Hospitalini, katika nyumba za uuguzi na vituo vya walezi, kufanya kazi kila wikendi ya pili mara nyingi ni lazima. Nafikiri wikendi zinapaswa kulipwa mara moja na nusu kama sikukuu.”

Kemi Omolaiye: “Kama Nigeria ingekuwa bora, je, angeenda ughaibuni kutafuta maisha bora? Inasikitisha sana. Nawahurumia familia changa iliyoachwa nyuma. Mwenyezi Mungu awafariji familia yote. Pumzika kifuani mwa Bwana, baba mwema.”

Umeh Stina: “Hatujali afya zetu. Ni watu wangapi wanaomwona daktari wao kwa uchunguzi wa kawaida na vipimo vya damu? Wengine hufanya kazi siku sita hadi saba kwa wiki bila kupumzika. Wengi hawawezi kuomba ruhusa ya ugonjwa kwa hofu ya kunyimwa marupurupu na zamu zao za ziada. Roho yake ipumzike kwa amani. Fanya kazi, pumzika, nenda likizo, na sikiliza mwili wako. Sawazisha kazi na maisha.”

Daado-Ouma Baldeh: “Kwa nini kusema msongo wa kiwango hicho si wa watu dhaifu? Nani alisema alikuwa dhaifu? Hata wenye nguvu wanaweza kuvunjika. Binadamu si mashine. Kijana huyo alikuwa na kila kitu kikienda sawa kwake. Sasa familia yake italazimika kuanza upya maisha yao. Inasikitisha sana. Mungu aipokee roho yake. Amina.”

Richmond Mensah alikuwa na umri wa miaka 33 alipofariki.
Richmond Mensah alikuwa babab wa watoto watatu. Picha: Fajira.
Source: Facebook

Muuguzi Mkenya anayeishi Uingereza apatikana amefariki

Pia soma

Lloyd Ochieng: Familia Yahuzunika baada ya Mwili wa Ndugu Yao Aliyepotea Kupatikana Msituni Ngong

Katika kisa kingine, muuguzi Mkenya anayeishi Uingereza alipatikana amefariki nyumbani kwake, hali iliyozua ghadhabu mtandaoni huku watu wakitaka majibu.

Mamlaka zilianzisha uchunguzi wa kina kuhusu kifo cha Peninah Muiruri na kupanga kufanyika kwa uchunguzi wa maiti.

Familia yake iliyogubikwa na huzuni iliomba msaada kwa umma ili kurejesha mwili wa binti yao nyumbani na kumpa mazishi yanayostahili.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *