- Salamu za rambirambi zinaendelea kumiminika kufuatia kifo cha kusikitisha cha Mbunge wa Emurua Dikirr, Johanna Ngeno, ambaye alifariki kwenye ajali ya ndege Februari 28
- Picha za mjane wa mbunge huyo akimwaga machozi bila kujizuia nyumbani kwao Karen ziliwafanya Wakenya kutokwa na machozi
- Picha za binti mkubwa wa Ngeno akiandika katika kitabu cha taabini za babake ziligusa wengi zaidi
Picha za binti mkubwa wa Johanna Ngeno akiandika katika kitabu cha taabini cha babake zimewaacha Wakenya wakiwa wamevunjika moyo.

Source: Facebook
Mbunge huyo wa Emurua Dikirr, ambaye alikuwa akitumikia mara yake ya tatu tangu achaguliwe 2013, Ngeno aliangamia katika ajali ya chopper iliyotokea saa 4:45 jioni mnamo Februari 28 katika eneo la Chepkiep eneo bunge la Mosop, Kaunti ya Nandi.
Kiongozi huyo wa Kipsigis alifariki pamoja na wengine watano, akiwemo mpiga picha wake, Nick Kosgei. Mpiga picha huyo mwenye umri wa miaka 25 alikuwa amebadilisha status yake ya WhatsApp dakika chache kabla ya saa moja usiku, saa tatu kabla ya kuanguka.

Pia soma
Johanna Ngeno: Babake Mpiga Picha Aliyeuawa Pamoja na Mbunge Afichua Mazungumzo yao ya Mwisho
Johanna Ngeno alikuwa na watoto wangapi?
Mbunge huyo wa Emurua Dikirr alikuwa na mke mmoja, Nayianoi Ntutu Ngeno, na walibarikiwa na wasichana wawili wa kupendeza.
Baba huyo mwenye upendo mara nyingi alichapisha kuhusu watoto wake, akawasherehekea, na chapisho lake la mwisho kuhusu malaika wawili wadogo lilikuwa Februari 22, wakati wa siku ya kuzaliwa ya mama yao.
Ngeno alichapisha video ya kupendeza ya mkewe, na watoto wao wawili wakati wa siku ya kuzaliwa ya Ntutu, akimtakia kila la heri.
Mume huyo aliyejaa mapenzi alionyesha upendo wake katika siku yake maalum. Katika video hiyo, mbunge huyo alimlisha mke wake keki kabla ya kuwalisha watoto wao na wanafamilia waliokuwepo.
Mwanamume huyo mwenye upendo kisha akampa Ntutu maua kabla ya kumbusu. Video hiyo alikuwa ameambatanisha na wimbo wa Otile Brown wa Chaguo la Moyo akimshirikisha Sanaipei. Video hiyo iliibuka tena baada ya kifo cha Ngeno, na kuwaacha Wakenya wakiwa na huzuni.
Mnamo Machi 1, waombolezaji walipomiminika nyumbani kwa Ngeno Nairobi Karen kufariji familia yake, kitabu cha taabini kiliwekwa nje ya nyumba yake, kikiwa na picha yake. Kwenye picha, mbunge huyo alikuwa amevalia mavazi ya asili ya kimasai.

Pia soma
Johanna Ngeno: Mkewe Mbunge Aonekana kwa Mara ya Kwanza baada ya Kifo cha Mumewe, Wakenya Wamfariji
Picha za binti wa kwanza wa Ngeno akiwa ameshika kalamu huku akiandika katika kitabu cha taabini ziliwagusa wengi.
Bila kujali kilichokuwa kikiendelea, msichana huyo alitabasamu huku akiandika kwenye kitabu hicho. Ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na mjane wa Ngeno aliyekuwa akihuzunika, huku akitokwa na machozi wanafamilia wakimfariji.
Mjane huyo mchanga, akiwa amevalia mavazi meusi, alitokwa na machozi kila wakati waombolezaji walipoingia nyumbani kumfariji. Picha hizo zilisambaa huku Wakenya wakiiombea familia hiyo changa.
Zifuatazo ni picha za binti wa Ngeno akiandika katika kitabu cha taabini cha baba yake:
Wakenya wamfariji bintiye Johanna Ngeno
Picha za msichana huyo zilisambaa mitandaoni, na kuibua hisia miongoni mwa Wakenya.
Carol Mitch alisema: “Inasikitisha sana roho hii mchanga haielewi kuwa baba yake amekwenda milele na harudi tena ðŸ˜ðŸ˜!”
Jemba Denis aliandika: “So sad. Hilo ni kiwewe cha maisha atakua nacho. 😪.”
Livingstone Chendany alisema: “Inasikitisha sana 😠na chungu.”
Milly Makinia alisema: “Mungu awafariji.”
Mess Dee aliandika: “Walaii huyu amenigusa 💔💔💔.”

Source: Facebook
Baba wa mpiga picha wa Johanna Ngeno azungumza
Katika hadithi nyingine, familia ya marehemu Nick Kosgei ilifichua kuwa walikuwa wameanza kufanya mipango ya maziko ya mwanahabari huyo.
Kosgei, ambaye alikuwa mpiga picha rasmi wa Johanna Ngeno, alifariki katika ajali hiyo ya kusikitisha pamoja na mbunge huyo na wengine wanne.
Akizungumza na Citizen TV, babake Kosgei, Phillip Kosgei, alikumbuka mazungumzo yao ya mwisho. Ijumaa, Februari 27, baba mwenye huzuni alimtumia Nick SMS yenye maelezo ya benki ili kumlipia dadake karo ya shule.
Phillip alikumbuka kujaribu kufuatilia asubuhi iliyofuata ili kuthibitisha kama ada hizo zililipwa na kupata hati ya benki.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
