Marekani imetangaza  vikwazo dhidi ya  jeshi la Rwanda na maafisa wake wanne wakuu.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Uamuzi huo ulitangazwa na Ofisi ya Udhibiti wa Mali za Kigeni ya Marekani kutokana na Usaidizi wa moja kwa moja wa operesheni wa Kigali kwa harakati za waasi wa M23 na washirika wake mashariki mwa DRC. Vikwazo hivi vilikuwa vimejadiliwa kwa karibu miezi miwili kulingana na Thomas Pigott, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani .

Hii inahusisha kufungiwa kwa mali nchini Marekani na marufuku ya miamala yoyote na watu binafsi au makampuni ya Marekani ispokuwa pekee kwa kwa mikataba au shughuli ambazo tayari zinaendelea, hadi Aprili 1, 2026.

Thomas Pigott, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani , alijaribu kuweka vikwazo hivi katika muktadha.

Siku chache tu baada ya kusainiwa kwa tamko linalohusiana na Makubaliano ya Washington, wapiganaji kutoka AFC/M23, wanaoungwa mkono na Rwanda, alielezea, walichukua udhibiti wa mji wa Uvira, hali ambayo amesema huu ni Ukiukaji wa wazi wa makubaliano haya.

Thomas Pigott alisisitiza kwamba M23 tayari ni chombo kilichowekewa vikwazo Na Marekani, Na Umoja wa Mataifa.

Kulingana na msemaji huyo, harakati hiyo inawajibika kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu mauaji ya jumla, unyanyasaji dhidi ya raia, wakiwemo wanawake na watoto.

Na ni msaada unaoendelea wa jeshi la Rwanda na amri yake kuu, alidai, ndio umeruhusu M23 kukamata maeneo huru nchini DRC na kuendelea na ukiukwaji huu.

“Hatua iliyotangazwa leo inaonyesha azimio la Marekani la kuunga mkono Makubaliano ya Washington.

Kwa upande wa Rwanda, Paul Kagame alikuwa wazi mwanzoni mwa Februari. aliposema “Vita nchini DRC havikuanzishwa na Rwanda, wala havikuanzishwa na Rwanda.” Kuhusu vikwazo, alisema tena kwamba hawezi kulea mikono vimuathiri.

Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu jioni, Kinshasa imeishukuru Marekani,” ikikaribisha uamuzi wa Washington

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *