
Utawala wa Trump umejaribu kujitetea kwa umaa siku ya Jumanne, Machi 3, kufuatia kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio ambaye alisema kuwa Marekani ilianzisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa kushinikizwa naIsrael. Matamshi haya yamezua gumzo nchini Maekani hasa kutoka kwa upinzani wa Democratic na wafuasi wa rais mwenyewe.
Imechapishwa:
Dakika 3 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Siku ya Jumanne, Donald Trump alitupilia mbali wazo kwamba Israel ilishinikiza Washington katika mgogoro huo, akibainisha kinyume chake. “Labda niliwashinikiwa wao,” alisema kuhusu Israel wakati alipokuwa akimpokea Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz katika Ikulu ya White House. “Tulikuwa tukijadiliana na wapumbavu hawa, na kwa maoni yangu, wangelianza kushambulia,” rais wa Marekani aliongeza kwa waandishi wa habari kuhusu Iran. “Kama tusingefanya hivyo, wangelianza kushambulia. Nilikuwa na uhakika na hilo.”
Marco Rubio aliwaelezea waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Marekani ilianza mashambulizi yake mapema Jumamosi asubuhi ili kukabiliana na “tishio lililokuwa karibu” la shambulio kutoka Iran. “Tulijua Israel ingechukua hatua. Tulijua kwamba hii ingesababisha shambulio dhidi ya vikosi vya Marekani, na tulijua kwamba ikiwa hatungevishambulia kabla ya kuanzisha mashambulizi hayo, tungepata hasara kubwa zaidi,” Rubio alisema siku ya Jumatatu. Alirudia maneno haya siku ya Jumanne mbele ya Bunge, wakati huo akiwafahamisha wanachama wote, akivituhumu vyombo vya habari kwa kupotosha matamshi yake na kukumbusha kwamba alisema operesheni hii “ilibidi ifanyike bila kujali” ili kuharibu uwezo wa makombora ya Iran. “Hapana, niliwaambia ilibidi ifanyike bila kujali,” alisema. Kuhusu muda wa mashambulizi, “rais alitenda kwa wakati ambao ulitupa nafasi nzuri ya kufanikiwa.”
Swali hili la “tishio lililo karibu” ndilo kiini cha mjadala kuhusu uhalali wa Donald Trump kuanzisha mgogoro huo. Upinzani wa Democratic umekasirishwa na uzinduzi wa mgogoro bila idhini ya bunge au mkakati uliofafanuliwa vizuri, ukibainisha kwamba maelezo ya Marco Rubio yalionyesha kwamba Israel “ilihatarisha vikosi vya Marekani kwa kusisitiza kushambulia Iran.”
Ukosoaji kutoka kwa mrengo wa kulia nchini Marekani
Wachambuzi kadhaa wakuu wa kihafidhina wameongeza ukosoaji wao kuhusu mashambulizi ya mabomu ya Marekani nchini Iran, wakibainisha kwamba maoni ya Marco Rubio yalionyesha kwamba Israel, na sio utawala wa Trump, ndiyo iliyokuwa ikifanya maamuzi. “Kwa hivyo kimsingi anatuambia kwamba tuko vitani na Iran kwa sababu Israel ilitulazimisha,” aliandika Matt Walsh, mtangazaji wa kipindi cha podikasti cha kihafidhina kinachofuatiliwa na watu milioni nne kwenye mtandao wa kijamii X, akimaanisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. “Hilo ndilo jambo baya zaidi ambalo angeweza kusema,” aliongeza kwenye mtandao wa kijamii wa X.
Hata kabla ya maoni ya Marco Rubio siku ya Jumatatu, sauti za kihafidhina zilionyesha kutokubali kampeni ya kijeshi iliyozinduliwa siku ya Jumamosi nchini Iran. “Kazi ya serikali yetu si kuangalia Iran au Israel. Ni kuangalia sisi wenyewe,” Megyn Kelly aliwaambia wasikilizaji wa kipindi chake, akibainisha mashaka yake kuhusu uamuzi wa Donald Trump. “Kwangu mimi inaonekana kama vita vya Israel.” “
Alikuwa mtu mashuhuri wa zamani katika harakati za Trump za MAGA (Make America Great Again), mbune wa zamani wa chama cha Republican Marjorie Taylor Greene alielezea masikitiko yake kwenye mtandao wa kijamii wa X kwamba “sasa tuko taifa lililogawanyika kati ya wale wanaotaka kwenda vitani kwa ajili ya Israel na wale wanaotaka amani tu na kuweza kulipa bili zao na bima yao ya afya,” miezi minane kabla ya uchaguzi muhimu wa katikati ya muhula mwezi Novemba.
Wakati wa kampeni yake ya ushindi ya mwaka 2024, Donald Trump aliweza kutegemea uungwaji mkono wa watu wenye msimamo mkali kutoka mrengo wa kulia waliotaka kukomeshwa kwa uingiliaji kati wa kijeshi wa Marekani nje ya nchi.
Ukosoaji huu kutoka kwa mrengo wa kulia wa Marekani unakuja huku maafisa waliochaguliwa wa Republican wakiwa na wasiwasi kuhusu athari za Vita vya Iran-Iraq kwenye uchaguzi ujao wa katikati ya muhula katika Bunge mwezi Novemba, ambapo chama hicho kinatarajia kudumisha wingi wake katika mabaraza yote mawili.
” Rais wa Marekani alijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari siku ya Jumanne kwa mara ya kwanza tangu kuzinduliwa kwa operesheni ya kijeshi kati ya Marekani na Israel nchini Iran siku ya Jumamosi. “Ilibidi ifanyike,” alisema, bila kuwahi kuelezea hapo awali, kabla ya Jumamosi, sababu za kwenda vitani dhidi ya Iran.