Matukio yasiyoeleeka yalmetokea Maiduguri siku ya Jumatatu jioni. Chini ya saa moja baada ya Waislamu kufturu, mji mkuu wa Jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria ulikumbwa na milipuko kadhaa. Hakuna kundi ambalo limedai kuhusika na mashambulizi hayo. Haya yalitokea saa 24 tu baada ya vikosi vya usalama vya pamoja kuzuia shambulio la usiku kwenye kambi ya kijeshi huko Ajilari, kitongoji cha Maiduguri ambapo kikosi cha wanajeshi kimewekwa.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Hali ni ya huzuni kutokana na majeruhi wengi,” daktari wa katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Maiduguri amemwambia mwandishi wetu huko Abuja, Moïse Gomis. Hata hivyo, ameongeza, hali “imedhibitiwa” kutokana na juhudi na mwitikio wa timu za matibabu za hospitali hiyo. Maiduguri inaonekana imeguswa kabisa. Mashahidi wengi waliripoti kusikia milipuko kadhaa iliyotokea kwa wakati mmoja Jumatatu, Machi 16, karibu saa 1:30 usiku kwa saa za Nigeria.

Maeneo matatu yameathiriwa

Maeneo matatu yameathiriwa katika mji mkuu wa Jimbo la Borno: ofisi kuu ya posta, Monday Market – moja ya masoko yenye shughuli nyingi zaidi Maiduguri – na Hospitali ya Chuo Kikuu cha Maiduguri, ambapo watoto wadogo wanaripotiwa kuwa miongoni mwa wengi waliojeruhiwa.

Ripoti ya awali ya polisi inabainisha kuwa watu 23 wamefariki na zaidi ya 100 wamejeruhiwa. Gavana wa jimbo hilo, Babagana Zulum, tayari amelaani mashambulizi hayo katika taarifa. Tukio hili la hivi karibuni la kusikitisha linakumbusha siku mbaya za katikati ya miaka ya 2010, zilizokubwa na wimbi la mabomu ya kujitoa mhanga yaliyodaiwa kwanza na Boko Haram, kisha na ISWAP.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *