
Rais wa Cuba Miguel Diaz-Canel ameahidi siku ya Jumanne, Machi 17, “upinzani usioweza usioweza kusababisha madhara” dhidi ya vitisho vya Donald Trump vya kutaka kuchukua udhibiti nchi hiyo.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Kutokana na hali mbayainayoweza kutokea, Cuba ina uhakika wa jambo moja: mchokozi yeyote wa nje atakabiliwa na upinzani usioweza kusababisha madhara,” Rais wa Cuba Miguel Diaz-Canel ametangaza kwenye mtandao wa kijamii wa X.
Siku ya Jumatatu, Donald Trump alisema “anaamini” kwamba “ikibidi ataichukua Cuba,” bila kutaja haswa alichomaanisha. Pia alizungumzia “kukikomboa” kisiwa hicho.
“Karibu kila siku, Marekani inatishia Cuba hadharani kwa kuipindua kwa nguvu utaratibu wake wa kikatiba. Wanatumia kisingizio cha kuchukiza: vikwazo vikali vilivyowekwa kwa uchumi dhaifu ambao wameushambulia na kujaribu kuutenga kwa zaidi ya miongo sita,” alishutumu rais wa Cuba, akimaanisha vikwazo vya Marekani vilivyowekwa tangu mwaka 1962.
“Wanatangaza mipango ya kuichukua nchi, rasilimali zake, mali zake, na hata uchumi wake—uchumi uleule wanaojaribu kuukandamiza ili kulazimisha kujisalimisha kwetu,” aliongeza Miguel Díaz-Canel, huku Washington ikiweka shinikizo kubwa kwenye kisiwa hicho kwa kuzuia usafirishaji wote wa mafuta.
“Ni kwa njia hii tu mtu anaweza kuelezea vita vikali vya kiuchumi vinavyoendeshwa kama adhabu ya pamoja dhidi ya raia wote wa Cuba,” aliongeza rais wa Cuba.
Kwa wiki kadhaa, Donald Trump amekuwa akitoa kauli kali zaidi dhidi ya Cuba na viongozi wake, huku akisisitiza kwamba kisiwa hicho, katika mazungumzo na Washington, kinataka “kufikia makubaliano” na Marekani.
Siku ya Ijumaa Cuba ilibainisha kwamba iko katika mazungumzo na jirani yake na kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa kama sehemu ya makubaliano yaliyosimamiwa na Vatican, mpatanishi wa muda mrefu kati ya mahasimu hao wawili wa kiitikadi.