Vita vipya vya maneno vimezuka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Rwanda katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Mnamo Aprili 15, hali mashariki mwa DRC, na kwa upana zaidi katika eneo la Maziwa Makuu, ilikuwa kwenye ajenda ya mkutano wa chombo cha Umoja wa Mataifa, na wawakilishi kutoka Kigali na Kinshasa walishutumiwa kila mmoja kwa kukiuka ahadi zao.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi

Nchi kumi na mbili kwa mara nyingine zimeitaka Rwanda kuondoa wanajeshi wake kutoka DRC. Lakini balozi wa Rwanda aliibua suala la tishio linaloendelea kutolewa kwa nchi yake na kundi la waasi wa Kihutu wa Rwanda la FDLR, ikundi lenye silaha amblo awali liliundwa na wahalifu wa zamani wa mauaji ya kimbari wa Rwanda.

“Hamna haki ya kuja kuwalinda raia wa Kongo katika ardhi yao.” “Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ina vifaa vya kutosha kuhakikisha usalama wa raia wake,” mwakilishi wa Kongo amejibu.

Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Maziwa Makuu kisha ametoa wito kwa pande zote kutekeleza usitishaji mapigano mara moja. “Hakuna suluhu, hakuna upatanishi, hakuna utaratibu wa uthibitishaji unaoweza kufanikiwa ikiwa pande husika moja kwa moja hazichagui njia ya amani,” ametangaza.

“Wale wanaoharibu amani watarajie madhara”

Hatimaye, Marekani imetoa wito kwa serikali ya Kongo kuheshimu ahadi zake za kuvunja FDLR mara moja. Na imeonya pande zote: “Wale wanaoharibu amani wanapaswa kutarajia madhara,” ameongeza balozi wa Marekani. Kama ukumbusho, Marekani iliweka mfululizo wa vikwazo dhidi ya Rwanda mwezi Machi mwaka huu.

Mashariki mwa Kongo, eneo lenye utajiri wa maliasili na linlopakana na Rwanda, limekuwa likikumbwa na vurugu kwa miaka 30. Makubaliano kadhaa ya kusitisha mapigano na mapatano yamesainiwa tangu mwishoni mwa mwaka 2021 na kuibuka tena kwa kundi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda.

Mapema mwaka wa 2025, AFC/M23 na washirika wake waliteka miji mikubwa ya Goma na Bukavu mfululizo baada ya mashambulozi makubwa.

Makubaliano mawili yamesainiwa tangu: tamko la kanuni huko Doha na AFC/M23 na serikali ya Kinshasa, likielezea ahadi za kusitisha mapigano, na makubaliano “ya amani na ustawi,” yaliyosainiwa mwezi Desemba huko Washington na DRC na Rwanda. Hadi sasa, nakala hizi mbili hazijakomesha mapigano hayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *