xcv

Chanzo cha picha, Getty Images

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Leo siku ya Alhamisi alilaani vikali mauaji ya waandamanaji nchini Iran, kufuatia ukosoaji kutoka kwa rais wa Marekani Donald Trump wiki iliyopita kwa madai kuwa hakuchukua msimamo huo wazi alipokuwa akizungumzia vita vinavyohusisha Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Akiwa papa wa kwanza kutoka Marekani, Leo pia alilaani vifo vya raia wengi katika mzozo huo na kueleza masikitiko yake kuhusu kuvunjika kwa mazungumzo ya amani kati ya Marekani na Iran.

Alitoa kauli hizo akiwa ndani ya ndege akirejea Roma baada ya ziara yake barani Afrika.

“Ninalaani vitendo vyote visivyo vya haki. Ninalaani kuuawa kwa watu,” alisema papa alipokuwa akijibu swali la waandishi wa habari kuhusu ripoti za kuuawa kwa waandamanaji nchini Iran.

Aliongeza kusema kuwa pale ambapo serikali au taifa linachukua maamuzi yanayosababisha vifo vya watu bila haki, hatua hiyo inapaswa kulaaniwa wazi.

Hapo awali, Aprili 12, Trump alimshambulia Papa Leo kupitia mitandao ya kijamii akimuita “asiyefaa,” baada ya kiongozi huyo wa kanisa Katoliki kuonekana kukosoa vikali vita vya Iran pamoja na sera za kupinga uhamiaji za rais huyo.

Katika chapisho lingine siku mbili baadaye, Trump alihoji ikiwa kuna mtu angemfahamisha Papa Leo kuhusu vifo vya waandamanaji nchini Iran.

Unaweza kusoma pia:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *