Nchini DRC, chama cha rais wa nchi hiyo UDPS kimefanya maandamano katika mitaa ya Kinshasa. Uhamasishaji huo ulikuwa wa kuunga mkono vikwazo vya Marekani vilivyomlenga rais wa zamani Joseph Kabila, aliyeshutumiwa na Washington na mamlaka ya Kongo kwa kuunga mkono Waasi wa AFC/M23 mashariki mwa nchi.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Chini ya urais wa Felix Tshisekedi, DRC ilihitimisha makubaliano ya madini na Marekani badala ya usaidizi wa usalama. Mkataba huu umekosolewa na upinzani, ambao unaona muunganiko huu wa kisiasa ukiwa umesalia miaka miwili katika muhula wa rais, huku kukiwa na tuhuma za kuwania muhula wa tatu kinyume na Katiba.

Maandamano hayo yalipangwa kuanza mapema asubuhi ya leo, Mei 4, 2026, lakini yalicheleweshwa na mvua. Muda mfupi kabla ya saa 5:00 asubuhi, maelfu ya waandamanaji walianza kumiminika kuelekea mtaa wa kwanza wa Lumumba katika mji mkuu wa DRC.

Chama cha UDPS hakikuwa pekee katika uhamasishaji huu, vyama vingi kutoka muungano tawala na wanachama wa kanisa la kiinjili walijiunga nao.

Waandamanaji walisikka wakilalamika “Kabila alidhibitiwa, Kabila alipunguzwa nguvu, Kabila atakamatwa hivi karibuni”

Baadhi walikuwa na bendera za vyama vyao au viongozi. Wengine, wakiwa wamevaa nguo nyeupe, waliinua mabango na mabango yaliyoonyesha ujumbe wa kuunga mkono Marekani.

Miongoni mwao alikuwa Mukendi, mtu mwenye umri wa miaka sitini akiwa amevaa bendera mbili za Marekani kichwani. “Ikiwa Donald Trump yuko pamoja nasi, ni nani atakayekuwa dhidi yetu?” alitangaza.

Kaulimbiu za Mabadiliko ya Katiba

Katikati ya maandamano hayo, kaulimbiu za kuunga mkono mabadiliko ya katiba pia zilisikika. “Lakini hiyo sio mada iliyo kwenye ajenda,” kiongozi wa chama, akiwa amezungukwa na wafuasi wake, alifafanua haraka.

Maandamano yalielekea Ikulu ya Watu. Ujumbe mdogo ulipangwa kwenda Ubalozi wa Marekani kuwasilisha hati yao na ambayo yaliyomo hayakuwekwa wazi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *