
Rais wa Angola Joao Lourenço amempokea Balozi James Swan, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkuu wa Ujumbe wa MONUSCO, Jumatatu, Juni 15, 2026. ofisi ya rais wa Angola iliripoti kwamba majadiliano hayo yalilenga hali ya usalama mashariki mwa DRC, katika muktadha unaoshuhudiwa na mwendelezo wa uhasama kati ya pande zinazozozana, pamoja na hali ilivyo katika upande wa kidiplomasia, haswa mchakato wa Washington na Marekani na mchakato wa Doha na Serikali ya Qatar.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Ingawa hayupo tena mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Joao Lourenço anaendelea kufuatilia kwa karibu hali hiyo. Mkutano huu ulimruhusu mkuu wa MONUSCO, akirudi kutoka Goma kwa mara ya pili tangu achukue madaraka, kuthibitisha tena kujitolea kwa Umoja wa Mataifa kuunga mkono utekelezaji na uthibitishaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano mashariki mwa DRC.
“Hali ya usalama katika nchi jirani ilitawala mkutano huo,” alisema mwanadiplomasia huyo, ambaye amekuwa akifanya kazi nchini DRC tangu mwezi Machi mwaka huu. Alibainisha, katika sehemu nyingine ya maoni yake, “ahadi ya Umoja wa Mataifa ya kuunga mkono utekelezaji na uthibitishaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano mashariki mwa Kongo,” ofisi ya rais wa Angola ilisema.
Wakati huo huo, ofisi ya rais wa Angola uliongeza, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mkuu wa MONUSCO, James Swan, alipongeza juhudi kubwa za Angola kwa miaka kadhaa kukuza amani, usalama, na utulivu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kiongozi mpya wa MONUSCO alichukua uongozi wa ujumbe huo kufuatia kuongezwa kwa muda wake wa mwaka mmoja na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, halali hadi Desemba 20, 2026. Atachukua jukumu zito la kutekeleza azimio la agizo hili jipya. Uamuzi huu unaojulikana kama Azimio 2808, unaeleza kwamba MONUSCO itadumisha idadi ya juu ya wanajeshi 11,500, waangalizi 600 wa kijeshi na maafisa kutoka mamakao makuu ya kikosi hiki, maafisa 443 wa polisi, na wanachama 1,270 wa vitengo vya polisi vilivyoundwa.
Vipaumbele vya kimkakati vya ujumbe huo ni: kuchangia katika ulinzi wa raia katika eneo ambapo wanajeshi wa ujumbe huo watatumwa; kufikia malengo yaliyowekwa na Azimio 2773 (2025); na kuimarisha na kudumisha taasisi za serikali nchini DRC.
Tofauti na maagizo ya awali, Azimio 2808 linabainisha kusitishwa kwa muda kwa zoezi la kuwaondoa wanajeshi wa MONUSCO taratibu, kutokana na kuzorota kwa hali ya usalama huko Ituri, Kivu Kaskazini, na Kivu Kusini, ambapo ujumbe huo una jukumu la kufuatilia usitishaji mapigano.
Likitetewa na Ufaransa, azimio hilo pia linajumuisha mifumo mipya ya kidiplomasia, haswa Mkataba wa Amani wa Washington (uliosainiwa mwezi Juni 2025 kati ya DRC na Rwanda) na Mkataba wa Amani wa Doha (Novemba 2025). Katika muktadha huu, MONUSCO inatakiwa kuchukua jukumu kubwa zaidi katika kusaidia usitishaji mapigano wa kudumu, haswa kupitia utaratibu wa ufuatiliaji na uhakiki.