Sandro Tonali,

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Iliyochapishwa

Muda wa kusoma: Dakika 3

Tottenham imejiunga katika ushindani na Arsenal pamoja na Manchester City kuwania saini ya kiungo wa Italia, Sandro Tonali, mwenye umri wa miaka 26. Newcastle inatarajiwa kutaka ada ya karibu pauni milioni 100 kwa ajili ya mchezaji huyo. (Telegraph)

Real Madrid inapanga kutoa pauni milioni 80 ili kumsajili beki wa kati wa Manchester City na Ureno, Ruben Dias, mwenye umri wa miaka 29. (Mirror)

Manchester United imeweka thamani ya pauni milioni 40 kwa mshambuliaji wa England, Marcus Rashford, mwenye umri wa miaka 28, lakini haitaki kumuona akijiunga na Liverpool au Manchester City. (ESPN)

Manchester United pia inawafuatilia wachezaji wa West Ham, Mateus Fernandes na Crysencio Summerville. Hata hivyo, West Ham inahitaji jumla ya pauni milioni 140 kwa ajili ya wote kiungo Fernandes (21) na winga Summerville (24). (Mail)

Arsenal imekubaliana masuala binafsi na kiungo wa Ufaransa, Manu Kone, lakini bado haijafikia makubaliano ya ada na Roma, ambao wanataka euro milioni 50 (pauni milioni 43.2) kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Gazzetta dello Sport)

Liverpool yamng’ang’ania Yan Diomande

Yan Diomande

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Liverpool inaendelea na juhudi za kumsajili winga wa Ivory Coast, Yan Diomande, mwenye umri wa miaka 19 kutoka RB Leipzig, huku kocha mpya Andoni Iraola akiridhia usajili huo. (Teamtalk)

Manchester City na Chelsea zimewasiliana na wawakilishi wa beki wa kulia wa Italia, Marco Palestra, mwenye umri wa miaka 21, lakini bado hazijaanza mazungumzo rasmi na Atalanta. (Sky Sport Italia)

Al-Hilal imefufua nia yake ya kumtaka mshambuliaji wa Brazil, Raphinha, mwenye umri wa miaka 29 kutoka Barcelona. Hata hivyo, mchezaji huyo hataki kujadili mustakabali wake hadi baada ya Kombe la Dunia. (Globo)

Everton inachunguza uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Ubelgiji, Lois Openda, mwenye umri wa miaka 26, kwa mkopo wenye kipengele cha kumnunua baadaye kutoka Juventus. (Football Insider)

Leeds United na Nottingham Forest nazo zimejiunga katika mbio za kuwania huduma za Openda. (Teamtalk)

Marseille iko tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya kiungo wa England, Angel Gomes, mwenye umri wa miaka 25. Coventry City na Hull City ni miongoni mwa klabu zinazomuwania mchezaji huyo aliyekuwa kwa mkopo Wolves msimu uliopita. (Teamtalk)

Madrid kumuachia Camavinga kutua Inter Milan?

Camavinga

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Inter Milan imekuwa klabu ya hivi karibuni kuonyesha nia ya kumsajili kiungo wa Ufaransa, Eduardo Camavinga, mwenye umri wa miaka 23 kutoka Real Madrid katika dirisha hili la usajili. (Mundo Deportivo)

Brighton haiko tayari kulipa pauni milioni 60 zinazohitajika na Tottenham kwa ajili ya beki wa Croatia, Luka Vuskovic, mwenye umri wa miaka 19 ambaye alicheza kwa mkopo Hamburg msimu uliopita. (Football Insider)

Tottenham imekataa ofa kadhaa kwa ajili ya mshambuliaji wa England, Will Lankshear, mwenye umri wa miaka 21. Spurs inataka pauni milioni 20 kumuachia mchezaji huyo anayefuatiliwa na Sporting. (Hayters)

Paris FC imeanza mazungumzo na kocha wa zamani wa Chelsea na Strasbourg, Liam Rosenior, kuhusu uwezekano wa kuchukua nafasi ya Antoine Kombouare iwapo ataondoka majira haya ya joto. (L’Equipe)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *