• Familia yafichua kilichomuua mwanajeshi wa Kenya Air Force siku 2 baada ya kurejea nyumbani kuwatembelea wazazi wake
  • Mwanajeshi wa Kenya Air Force, Kevin Havi Adoli, alifariki dunia siku mbili tu baada ya kurejea nyumbani kuwatembelea wazazi wake katika Kaunti ya Vihiga
  • Mama yake alimkuta akiwa amepoteza fahamu akiwa ameketi kwenye kiti asubuhi ya Juni 10 na kumkimbiza hospitalini, ambako alitangazwa kufariki dunia

Uchunguzi wa maiti uliofanywa katika Mashujaa Memorial Funeral Home ulifichua chanzo cha kifo chake cha ghafla.

Kevin Havi aliaga dunia kutokana na kupasuka kwa aorta.
Familia ya Vihiga inaomboleza kifo cha Kevin Havi, askari wa Jeshi la Wanahewa la Kenya. Picha: Gerishom Andani.
Source: Facebook

Mjomba wake, Gerishom Andani, alishiriki matokeo ya uchunguzi huo pamoja na tarehe ya mazishi yake.

Familia ya mwanajeshi wa Kenya Air Force, Kevin Havi Adoli, imetangaza chanzo cha kifo chake baada ya uchunguzi wa maiti kufanyika.

Havi alifariki kwa huzuni kubwa alipokuwa akiwatembelea wazazi wake katika Kijiji cha Gimariani, Wadi ya Tambua, Eneo Bunge la Hamisi, Kaunti ya Vihiga.

Alikuwa ametumia siku mbili pekee nyumbani na alikuwa akijiandaa kuanzisha mradi uliolenga kuwasaidia wazazi wake na kuboresha maisha yao kabla ya mkasa huo kutokea.

Pia soma

Bintiye Angela Chibalonza Aendeleza Urithi wa Mamake, Aduwaza Watu Kanisani kwa Sauti Tamu

Mama yake mwenye majonzi alimkuta akiwa amepoteza fahamu kwenye kiti asubuhi ya Juni 10 alipokwenda kumwita kwa ajili ya kifungua kinywa.

Kwa bahati mbaya, alitangazwa kufariki dunia alipowasili katika Hospitali ya Aga Khan mjini Kisumu.

Ripoti ya uchunguzi wa maiti ilifichua nini kuhusu kilichomuua Kevin Havi?

Akizungumza na TUKO.co.ke, mjomba wa Havi, Mchungaji Gerishom Andani wa Pentecostal Assemblies of God, alishiriki matokeo ya uchunguzi wa maiti pamoja na mipango ya mazishi ya mwanajeshi huyo.

Gerishom alisema uchunguzi wa maiti ulifanyika Jumanne, Juni 16, katika Mashujaa Memorial Funeral Home.

“Kwa huzuni kubwa, tunatangaza kifo cha mwana wetu mpendwa, kaka, mume na mpwa wetu, Kevin Havi. Uchunguzi wa maiti ulifanyika katika Mashujaa Memorial Funeral Home, mochari ya Jeshi la Kenya, mbele ya wanafamilia akiwemo baba yake, mke wake, mjomba, shangazi, ndugu zake na binamu yake, pamoja na maafisa wa Jeshi la Kenya,” sehemu ya taarifa iliyoshirikiwa na Gerishom ilisoma.

Kulingana na matokeo ya uchunguzi huo, kijana huyo aliyekuwa na matumaini makubwa alifariki kutokana na kupasuka kwa aota.

Matokeo hayo yalitolewa wakati ambapo watu wengi walikuwa wakikisia chanzo cha kifo chake, huku baadhi wakihusisha kifo hicho na uchawi pamoja na madai mengine ambayo hayakuwa yamethibitishwa.

Pia soma

Magazetini: Ushindi Mkubwa kwa Sifuna! baada ya Gavana Kang’ata Kujiunga na Linda Mwananchi

Matokeo ya uchunguzi wa maiti sasa yameondoa uvumi huo wote na kufichua chanzo halisi cha kifo cha mwanajeshi huyo kijana.

Mwanajeshi wa Kenya Air Force atazikwa lini?

Familia ilimomboleza Havi kama mwanachama mpendwa na wa thamani mkubwa kwa familia na jamii kwa ujumla. Pia waliwashukuru wote waliokuwa pamoja nao katika kipindi hiki kigumu wanapojiandaa kumpa mazishi ya heshima.

Aidha, mchungaji huyo alitangaza kuwa mpwa wake atazikwa Jumamosi, Juni 27, nyumbani kwao Vihiga, akiongeza kuwa familia itatoa taarifa zaidi baadaye.

“Tunaomba muendelee kutuombea na kutuunga mkono tunapomwomboleza. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele,” familia ilisema.

Peter Karari alifariki vipi?

Katika habari nyingine, TUKO.co.ke iliripoti kuwa mwigizaji wa Kikuyu, Peter Karari, maarufu kama Gacheru au Raray, alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Madaktari waligundua uvimbe mkali wa ubongo (brain tumour) kupitia uchunguzi wa MRI, siku chache baada ya kipimo cha CT Scan kuonyesha kuwa hakukuwa na tatizo kubwa.

Mashabiki walimwomboleza kwa kushiriki picha za kugusa hisia kutoka siku yake ya harusi, huku wengi wakituma salamu za pole na faraja kwa mjane wake na familia yake.

Pia soma

Askari wa Jeshi la Anga la Kenya Afariki Siku 2 Baada ya Kurudi Nyumbani Kuwatembelea Wazazi Wake

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *