• Mwandishi huyo wa habari alimomboleza kwa hisia, akikumbuka uchangamfu wa mama yake wa kambo na upendo wake kwa maisha
  • Aliyekuwa mtangazaji wa Citizen Radio, Jeridah Andayi, ameshiriki ujumbe wa kuhuzunisha wa kumuenzi mama yake wa kambo, Mama Sarah
  • Mwandishi huyo wa habari anayeishi Marekani alimwelezea kama mwanamke mwenye upendo, hekima na uchangamfu ambaye alicheza nafasi maalum katika maisha yake

Aliyekuwa mtangazaji wa Citizen Radio, Jeridah Andayi, ameshiriki ujumbe wa kuhuzunisha wa kumuenzi mama yake wa kambo, Mama Sarah.

Jeridah Andayi akiwa amevaa hijabu ya bluu na mama yake(mchoro).
Jeridah Andayi akimlilia Mama yake wa Kambo, Mama Sara. Picha: Jeridah Andayi.
Source: Instagram

Mwandishi huyo wa habari anayeishi Marekani alimwelezea kama mwanamke mwenye upendo, hekima na uchangamfu ambaye alicheza nafasi maalum katika maisha yake.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Jeridah alimtambulisha Mama Sarah kama mmoja wa mama katika familia yao kubwa.

“Kutana na mama yangu. Mwingine tena. Huyu ni Mama Sarah. Ndoto ya baba yangu ilikuwa kuwa na familia kubwa. Kwa hivyo akajitafutia zaidi ya mama mmoja kwa watoto wake. Jamaa huyo alikuwa mjanja,” aliandika.

Pia soma

Kirinyaga: Mvulana wa Darasa la 8 Amtambua Mshukiwa Aliyemuua Mamake kwa Deni la KSh 500

Mwandishi huyo alitafakari kuhusu muundo wa kipekee wa familia yao, akibainisha kuwa ingawa alikuwa na mama yake mzazi, pia alikulia akiwa na mama wengine waliowapenda na kuwalea watoto wote kama wao wenyewe.

“Mama yangu alikuwa wa kwanza. Kisha akaja Mama Sarah. Huyu ndiye mwenye furaha. Yule anayekufundisha kwa siri jinsi ya kutoroka baada ya kufanya utundu mdogo mdogo,” alikumbuka.

Jeridah Andayi Alimwombolezaje Mama Sarah?

Jeridah alimwelezea Mama Sarah kama mwanamke ambaye hakuwahi kuwahukumu vijana, bali aliwaongoza kwa hekima na uelewa.

“Mahusiano yetu yalikuwa tofauti. Ulikuwa na mama yako mzazi, halafu ulikuwa na mama wengine. Ni kitu kilekile. Mama yangu alikuwa wa kwanza. Kisha Mama Sarah. Huyu ndiye mwenye furaha. Yule anayekufundisha kwa siri jinsi ya kutoroka baada ya kufanya utundu mdogo mdogo. Yule unayemtambulisha mpenzi wako wa ujana. Hatakuhukumu. Atamfanyia uchunguzi wa kina huyo kijana kisha akupe ripoti kamili. Anahitaji tu jina lake na jina la mzazi wake. Yeye atajua mengine yote. Kila undani mdogo,” alisema.

Kulingana naye, Mama Sarah alijua karibu kila kitu kinachoendelea kijijini na mara nyingi alikuwa mtu ambaye wakazi walimgeukia kwa ushauri na suluhisho.

“Mama anajua kila kitu kijijini. Anajua nani alifanya nini, wapi, kwa nini na vipi. Kila kitu kiko kwenye vidole vyake. Pia ni kama mzee wa kijiji. Anajua jinsi ya kushughulikia matatizo. Yeye ni mfanyakazi wa afya ya jamii. Anaangalia mtoto akiwa kwenye umati na anajua hajapata chanjo zake. Anaona mama mjamzito na anajua haendi kliniki zake za ANC. Anaijua kijiji kizima. Na hata zaidi,” alisema.

Pia soma

Marya Prude Acheka Kwa Kejeli Baada ya Ivy Namu Kutangaza Kuachana na Willis Raburu

Mbali na huduma zake kwa jamii, Mama Sarah alijulikana kwa misingi yake rahisi lakini thabiti ya maisha.

“Yeye ni aina ya mtu anayesafisha sufuria zake kwa waya wa chuma na kuziacha juani zikauke. Anaishi peke yake. Katika nyumba yake ndogo. Karibu na kituo cha biashara cha kijijini. Dada zangu wote wameondoka nyumbani. Lazima ale chakula kizuri. Haijalishi hana pesa kiasi gani… hatakula sukuma wiki bila kitu cha kuandamana nayo,” alisema.

Baadaye, ujumbe huo uligeuka kuwa wa huzuni kubwa huku Jeridah akijaribu kukubali ukweli wa kumpoteza mama huyo.

“Vipi? Mama anapenda maisha yake. Huyu mke wa baba yangu. Huyu ndiye mama wa dada zangu. Mama wa mtoto wa mwisho wa familia ya Andayi. Mwanamke huyu mrefu, mweusi na mrembo. Amekataa kuamka. Amelala baridi. Oohhh, Mama Sarah! Binti ya Emisiko. Namkunda. Polis. Ninakuomboleza mama,” aliongeza.

Mama Sarah akiwa ameketi.
Mama Sarah ni mama wa kambo wa Jeridah Andayi. Picha: Jeridah Andayi.
Source: Facebook

Jeridah Andayi Azungumzia Kumkosa Mama Yake Marehemu

Katika habari inayohusiana, Jeridah Andayi alisema anamkosa mama yake marehemu, akisema kuwa kadri mtu anavyozeeka ndivyo thamani ya mama inavyoongezeka.

Akizungumza kupitia mitandao yake ya kijamii, alikumbuka kumbukumbu zake na mama yake tangu kipindi cha ujana wake.

Pia soma

Mkenya aliyedhaniwa amekufa nchini UAE apatikana hai baada ya karibu mwaka mmoja: “Alituma salamu”

Alisema kuwa hatua muhimu za maisha kama ukuaji binafsi, kuwa mama na ndoa huchochea hamu ya kupata tena uhakikisho, mwongozo na ushauri wa wazazi.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *