• Mbunge wa Kuresoi Kaskazini, Alfred Mutai, anadaiwa kufyatua risasi katika Shule ya Sekondari ya Umoja Tulwet baada ya vurugu kuzuka mara alipowasili katika eneo hilo
  • Mbunge huyo alikuwa akihudhuria hafla ya uwezeshaji iliyoandaliwa na Gavana wa Nakuru, Susan Kihika, ambaye pia alikuwa na wafuasi wake katika mkutano huo
  • Mvutano uliongezeka baada ya basi la kikundi cha ustawi kuchomwa moto na gari la mbunge huyo kupigwa mawe

Watu watatu walijeruhiwa katika Shule ya Sekondari ya Umoja Tulwet, Kuresoi Kaskazini, Kaunti ya Nakuru, baada ya Mbunge wa eneo hilo Alfred Mutai kudaiwa kufyatua risasi.

Nakuru chaos
Nakuru: Tension as MP Fires Gunshots at School, 3 Injured
Source: Original

Kwa mujibu wa mashuhuda, Mutai aliwasili katika eneo la programu ya uwezeshaji ya leo iliyoandaliwa na Gavana wa Nakuru, Susan Kihika, akiwa ameandamana na mamia ya wafuasi wake.

Katika vurugu zilizofuata, mbunge huyo anadaiwa kufyatua risasi na kuwajeruhi baadhi ya wakazi waliokuwa wakijaribu kuwazuia yeye na wafuasi wake kuingia katika eneo la hafla hiyo.

Job Kiprono, mmoja wa wakazi wa eneo hilo, alipata jeraha la risasi kwenye mkono wake wa kulia wakati wa makabiliano hayo.

Pia soma

Kirinyaga: Mvulana wa Darasa la 8 Amtambua Mshukiwa Aliyemuua Mamake kwa Deni la KSh 500

Waliojeruhiwa walikimbizwa mara moja katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Molo ambako walipatiwa matibabu na wahudumu wa afya.

Miongoni mwa wengine waliojeruhiwa katika vurugu hizo ni Isaac Cheruiyot.

Hata hivyo, dakika chache baadaye, wafuasi wanaodaiwa kuwa wa mbunge huyo walichoma basi la kikundi cha ustawi cha Ngata Welfare Group.

Polisi walilazimika kufika eneo la tukio haraka na kuwatawanya huku gari hilo likiteketea kabisa kwa moto.

Katika eneo la hafla hiyo, usalama uliimarishwa huku kikosi cha maafisa wa polisi kikipelekwa kutoa ulinzi wa ziada.

Jana, Mutai alitembelea eneo hilo akiwa ameandamana na wafuasi wake na kuahidi kuhudhuria hafla hiyo.

Mutai na Gavana wa Nakuru, Susan Kihika, wamekuwa katika mvutano wa kisiasa kwa miaka kadhaa sasa, na mikutano ndani ya eneo bunge hilo imekuwa ikigubikwa na hali ya taharuki.

Akizungumza katika hafla hiyo, Susan Kihika alisema kuwa waliojeruhiwa wamepatiwa matibabu katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Molo na hali yao inaendelea kufuatiliwa; na iwapo itahitajika, watahamishiwa katika Nakuru County Teaching and Referral Hospital kwa matibabu ya kina zaidi.

“Kilichotokea leo asubuhi ni jambo la kusikitisha; ninakilaani na sitatishwa na mtu yeyote kuendesha mikutano yangu,” alisema.

Pia soma

Simanzi Kubwa: Wanandoa wa Thika na Wanao Wawili Waagwa kwa Uchungu

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Allan Chesang, Betty Maina, Rahab Mukami, David Gikaria, Irene Njoki na aliyekuwa Gavana wa Bomet pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Huduma za Mahakama, Isaac Rutto, miongoni mwa wengine.

Habari zaidi zinafuata…

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *