- Rachel Otuoma amesimulia jinsi alivyonusurika baada ya gari lililokuwa likiendeshwa kwa mwendo kasi kupoteza mwelekeo na kugonga magari kadhaa kwenye Nairobi Expressway
- Mwanamitandao wa TikTok alishiriki picha za gari lake aina ya Honda Vezel lililoharibika vibaya, akisema anashukuru kwa kunusurika ajali hiyo ya kutisha
- Rachel alisema alitoka kwenye ajali hiyo akiwa na maumivu madogo ya kifua na uchovu pekee, huku akimshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake licha ya ukubwa wa ajali hiyo
TikToker, Rachel Otuoma, amewahakikishia mashabiki wake kuwa yuko salama baada ya kunusurika ajali ya kutisha ya barabarani kwenye Nairobi Expressway.

Source: Instagram
Rachel, mjane wa aliyekuwa mwanasoka maarufu wa Kenya, Ezekiel Otuoma, alizungumzia tukio hilo wakati wa matangazo ya moja kwa moja kwenye TikTok, ambapo pia alishiriki picha za gari lake lililoharibika.
Rachel Otuoma alipatwa na nini?
Kulingana na Rachel, ajali hiyo ilitokea baada ya gari lililokuwa likiendeshwa kwa mwendo kasi kupoteza mwelekeo na kuingia katika njia aliyokuwa akiendeshea kabla ya kuligonga kwa kulikwaruza upande wa gari lake.
Alieleza kuwa alikuwa akiendesha kwenye Nairobi Expressway alipoliona gari hilo likimjia kwa kasi kubwa, na kwa haraka akalikwepesha gari lake kuelekea pembeni mwa barabara ili kuepuka kugongana uso kwa uso.
“Nilipoona lile gari likinijia, nililikwepa. Walikwaruza upande wa gari langu, lakini nyuma yangu hali ilikuwa mbaya kwa sababu waligonga magari manne. Siwezi hata kueleza nilivyoweza kusimama baada ya hapo. Magari yaliyokuwa mbele yangu yote yalikuwa yamefunguka mifuko ya hewa (airbags). Tangu nianze kuendesha gari, sijawahi kuona kitu kama hicho.”
Baadaye Rachel alishiriki picha za tukio hilo, zikionyesha mabaki ya gari lake aina ya Honda Vezel, ambalo alikuwa amelionyesha kwa fahari mtandaoni zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Alisema hata mashuhuda walishangazwa na jinsi alivyonusurika akiwa na majeraha madogo pekee licha ya ukubwa wa ajali hiyo.
“Nina bahati sana kwamba gari langu liliguswa tu upande wa abiria wa mbele. Ni Mungu. Gari langu sasa liko gereji. Kilicho muhimu ni maisha; kuhusu gari tutajali baadaye.”
Rachel aliongeza kuwa alipata uchovu na maumivu madogo ya kifua, lakini kwa ujumla yuko salama na anashukuru kuondoka kwenye ajali hiyo akiwa hai.
Tazama video hapa chini:
Wanamitandao waonyesha hisia zao

Pia soma
Mwanamke adai aliteseka Jehanamu kwa siku 18, akafichua aliyoyaona kabla ya kuamka hospitalini
Baada ya kusimulia mkasa huo, mashabiki wengi walifurika kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii wakimtumia ujumbe wa pole, maombi na maneno ya kumtia moyo baada ya kuona gari lake lilivyoharibika.
Haya ni baadhi ya maoni yao:
Brenda: “Pole, hiyo inatisha sana.”
PRECIOUS GRACIOUS: “Pole sana, Mungu akufunike na damu yake.”
JONASi: “Mungu aendelee kukulinda.”
Eunice: “Pole sana, Mungu akulinde.”
Vanessa: “Pole mama, Mungu anakupenda.”
Margaret Imbusi: “Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai. Pole kwako na wengine wote.”
Nyar Koma: “Gari linaweza kutengenezwa, lakini maisha ni ya thamani. Hilo linasikika la kutisha sana. Tunakuombea upone haraka. Tunamshukuru Mungu kwa kunusurika kwenye ajali hiyo mbaya.”

Source: Facebook
Je, Rachel Otuoma alipata mpenzi mwingine?
Hapo awali, TUKO.co.ke iliangazia taarifa kuhusu Rachel baada ya kufunguka kuhusu uhusiano wake miezi kadhaa baada ya kudai kuwa aliolewa tena kwa siri.
Kauli yake ya wazi kuhusu mapenzi na safari yake ya kihisia tangu kumpoteza mume wake wa kwanza imezua mjadala kuhusu mapenzi, maombolezo na matarajio ya jamii kuhusu kuoa au kuolewa tena.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
