
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Tanzania.
Taarifa za uteuzi huo zilitolewa Alhamisi na Spika wa Bunge, Mussa Zungu. Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Nchemba alikuwa Waziri wa Fedha, nafasi aliyokuwa nayo tangu mwaka 2021.