Ukiukwaji wa haki za binadamu unaripotiwa kuongezeka tena nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Ofisi ya Pamoja ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imechapisha mahitimisho yake kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2025: ongezeko la 11% la ukiukwaji ulioandikwa na ongezeko la 12% la waathiriwa ikilinganishwa na miezi sita iliyopita. 

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ripoti hiyo pia inaonya kuhusu upanuzi wa mgogoro mashariki mwa DRC, mbali na mokio ya Kivu Kusini na Kivu Kaskazini, pamoja na mienendo mipya na idadi kubwa ya maeneo yaliyoathiriwa.

Huko Ituri, mko unaopatikana kaskazini mashariki mwa DRC, vurugu hazipungui; kinyume chake, zinaongezeka. Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, ukiukwaji wa sheria za kimataifa za kibinadamu katika mkoa w Ituri umeongezeka kwa 21% ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.

Na mhusika mmoja anajitokeza katika tathmini hii: wapiganaji wa ADF. wapiganaji hawa wanaaohusishwa na kundi la kigaidi la Islamic State, walihusika na visa 198vya ukiukwaji wa haki za binadamu huko Ituri na Kivu Kaskazini, huku waathiriwa angalau 1,071 wakirekodiwa katika miezi sita ya kwanza ya mwaka pekee.

Kwa maneno mengine, licha ya hali ya kuzingirwa kutangazwa na Kinshasa na operesheni za pamoja na jeshi la Uganda, ADF inabaki kuwa miongoni mwa makundi hatari zaidi.

Mgogoro unaozidi kuwa mgumu

Lakini sio wao pekee. Huko Ituri, mashambulizi pia yanaongezeka na makundi ya CODECO, kundi la Zaïre, na hata makundi mapya, kama CRP ya Thomas Lubanga, au au kundi la CNLC. Kwa kuibuka kwa makundi na wahusika wapya, pamoja na waathiriwa zaidi, mzozo unazidi kuwa mgumu.

Kilichoongezwa kwenye hili ni janga lingine: unyanyasaji wa kijinsia unaohusiana na migogoro. Kati ya mwezi Januari na Juni, waathiriwa 266 walirekodiwa, zaidi ya mara mbili ya idadi kutoka mwaka uliopita.

Vitendo vingi vya vurugu hivi vilifanywa katika mkoa wa Kivu Kaskazini, ukifuatiwa na mkoa wa Ituri, kisha mk  a Kivu Kusini na Maniema (Kati-Mashariki). Wahalifu hasa ni makundi yenye silaha: AFC/M23 inatajwa kwa waathiriwa 63, Codeco kwa waathiriwa 52, na kisha makukundi mbalimbali ya Mai-Mai.

Lakini Umoja wa Mataifa pia unawanyposhea kidole cha lawama maafisa wa serikali: jeshi na polisi. Na picha hii imethibitishwa.

Katika ripoti tofauti ya mwezi uliopita pekee, Kipimo cha Usalama cha Kivu kilirekodi mapigano 145 . AFC/M23 inahusika katika mapigano 89 kati yao. Mapigano yameongezeka licha ya mipango ya amani kati ya kundi hili la kisiasa na kijeshi na Kinshasa. Na, kulingana na ripoti hiyo, AFC/M23 ilikuwa kundi lenye vurugu zaidi mwezi Oktoba, la pili kwa ADF, ambalo liliwaua raia 75.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *