Picha ya mfano ya pamoja ilipigwa Washington na marais wa Rwanda na Kongo. Walialikwa Marekani na Donald Trump ili kuidhinisha kile kinachojulikana sasa kama “Mikataba ya Washington ya Amani na Utulivu.” Sherehe hiyo ilihudhuriwa na wakuu wengine kadhaa wa nchi kutoka bara la Afrika hususan: Burundi, Kenya, Angola, na Togo. Hata hivyo, hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) bado ni ya wasiwasi.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ilichukua karibu mwaka mmoja kufikia utiaji saini huu. Mwaka mmoja tangu mkutano ulioshindwa huko Luanda, Angola, ambapo wakuu hao wawili wa nchi walitakiwa kujitolea kwa tamko la pamoja. Sasa, changamoto ni kujaribu kutekeleza Mikataba hii ya Washington, anaripoti mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi.

Kupungua kwa mapigano bado si kweli. Kama uthibitisho, mapigano makali yaliripotiwa katika siku za hivi karibuni katika mkoa wa Kivu Kusini. Mapigano haya yamesababisha tena watu kuhama makazi yao.

Lakini makubaliano yaliyosainiwa hayana mifumo ya kufungamana. Kwa mfano, hakuna vikwazo vilivyowekwa kwa kutotekelza ahadi hizi, na nchi zote mbili bado zinaweka masharti ya utekelezaji wa makubaliano haya kwa masharti ya awali: kuvunjwa kwa kundi la waasi wa Kihutu wa Rwanda (FDLR) upande wa Kigali na kuondolewa kwa wanajeshi wa Rwanda katika ardhi ya DRC upande wa Kinshasa. “Tuko macho, lakini hatujakata tamaa,” rais wa Kongo hata hivyo alitangaza, huku mwenzake wa Rwanda akionya: “Ikiwa makubaliano haya yatashindwa, itakuwa kosa letu. Ni juu yetu, Afrika, kufanya kazi ya kuimarisha amani hii.”

Aina tatu za mikataba yasainiwa

Hakukuwa na kukumbatiana, wala kupeana mikono kati ya Félix Tshisekedi na Paul Kagame. Lakini wawili hao walisaini aina tatu za makubaliano huko Washington ambayo yanaunda mfumo kamili wa mchakato huo. Ili kuyaelewa kikamilifu, fikiria ngazi tatu. Ngazi ya kwanza ni makubaliano ya amani. Inajumuisha makubaliano ambayo tayari yalianzishwa katika miezi ya hivi karibuni. Lengo lake, kama Donald Trump mwenyewe alivyorudia, ni “kumaliza moja ya migogoro mirefu zaidi duniani.”

Kulingana naye, kifurushi hiki cha usalama kinajumuisha usitishaji mapigano wa kudumu, kupokonya silaha vikosi visivyo vya serikali, na vifungu vya kuruhusu wakimbizi kurudi nyumbani. Hiki ndicho kitovu cha ujenzi wa kisiasa na kijeshi: kile kinachokusudiwa kukomesha vita kati ya DRC na Rwanda.

“Kila mtu atapata pesa nyingi”

Ngazi ya pili ni mfumo wa ujumuishaji wa kiuchumi. Huu ndio uti wa kiuchumi wa mchakato huo. Wazo ni kufungua, kwa maneno ya Donald Trump, “enzi mpya ya maelewano na ushirikiano” kati ya Kinshasa na Kigali, kwa kushughulikia kile ambacho kimechochea mzozo kwa miongo kadhaa: kutoonekana kwa vituo muhimu vya usambazaji wa madini. Kwa hivyo mfumo huu unalenga kupanga upya vituo hivi vya thamani kwa njia ya uwazi, rasmi, na iliyodhibitiwa.

Ngazi ya tatu ina makubaliano ya pande mbili. Kuna mawili: moja kati ya Kinshasa na Washington, na jingine kati ya Kigali na Washington. Donald Trump alifupisha hoja yao kama ifuatavyo: “Kuna utajiri mkubwa katika nchi hii nzuri.”

Mikataba hii inalenga kufungua fursa mpya kwa Marekani kupata madini muhimu. Rais wa Marekani aliahidi kutuma “makampuni makubwa ya Marekani katika nchi zote mbili. Tutatoa baadhi ya madini adimu … na kulipa.” “Kila mtu atapata pesa nyingi,” alitangaza. Ushirikiano huu pia utashughulikia nishati, usafiri, na sekta zingine za kimkakati.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *