Siku ya Jumanne, katika mkutano wa televisheni wa baraza la mawaziri, alijibu taarifa za madai ya udanganyifu serikalini miongoni mwa baadhi ya wanajamii wa Kisomali kwa kuwaita wahamiaji hao “takataka” na kusema anataka warudishwe “walikotoka.”

Hotuba za kupinga uhamiaji zilikuwa sehemu kubwa ya kampeni ya Trump. Tangu aingie madarakani Januari, ameongoza oparesheni kali za maafisa wa serikali kii waliojificha uso kote nchini, akilenga kuongeza kuwarudisha wahamiaji makwao. Kadiri muda unavyosonga, lugha anayoyatumia hadharani kuhusu wahamiaji imekuwa kali zaidi.

Msako wa New Orleans

Vile vile siku ya Alhamisi, maafisa wa serikali kuu walisema wamekamata makumi ya watu huko New Orleans, jiji jingine linaloongozwa na Democrats.

Siku ya pili ya oparesheni ya New Orleans, waandamanaji walivuruga kikao cha baraza la jiji wakidai madiwani watangaze maeneo ya jiji kuwa “maeneo yasiyo na ICE,” ambako maafisa wa uhamiaji wa serikali kuu hawataruhusiwa kufanya shughuli za kuwakamata wahamiaji.

Waandamanaji walituhumu maafisa wa serikali kuu kuwajeruhi au kuwalenga watu wa rangi bila kubagua, wakiwemo raia wa Marekani wasiokuwa na rekodi ya makosa ya jinai—mashitaka ambayo DHS imeyakanusha.

Meya mteule wa New Orleans, Helena Moreno, alisema Jumatano kwamba oparesheni hiyo imeleta hali ya hofu miongoni mwa wakazi walio hatarini zaidi.

“Lazima tufanye yote tuwezayo kulilinda jiji la New Orleans na kuhakikisha kuwa mchakato wa haki unafuatwa kwa wakazi wote,” alisema, akitangaza mfumo wa mtandaoni kwa raia kuripoti unyanyasaji wa maafisa wa uhamiaji.

Gavana wa Louisiana, Jeff Landry, kutoka chama cha Republican, ameunga mkono juhudi za utekelezaji wa sheria za uhamiaji za serikali kuu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *