Msemaji wa kikosi hicho Jack Ombaka ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa kikosi hicho kimeimarishwa kuanzia mwezi Februari mwaka huu na kwamba kwa sasa kina jumla ya mafisa wapatao 980 huku idadi iliyokuwa ikitarajiwa awali ikiwa ni maafisa 2,500.

Kenya ndio imetuma maafisa wengi zaidi lakini Jamaica, Bahamas, Belize, Guatemala na El Salvador pia zimetuma askari. Magenge ya uhalifu nchini Haiti  yamekuwa yakiendesha mauaji, ubakaji na uporaji, katika mzozo mkubwa uliopelekea takriban watu milioni 1.4 kuyakimbia makazi yao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *