Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu atakutana na Rais wa Marekani Donald Trump mnamo Desemba 29 kujadili hatua zinazofuata za kusitisha mapigano Gaza, msemaji wa serikali ya Israel amesema siku ya Jumatatu Desemba 8.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Siku ya Jumapili, Netanyahu alisema kwamba atajadiliana na Trump kuhusu awamu ya pili ya mpango wa Marekani wa kukomesha vita huko Gaza baadaye mwezi huu. Usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas ulianza kutekelezwa mnamo mwezi Oktoba.

Pande zote mbili zimeshutumiwa mara kwa mara kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano na mapengo mapana yanabaki kwenye masuala muhimu ambayo bado hayajajadiliwa chini ya mpango wa Trump wa kukomesha vita, ikiwa ni pamoja na kupokonya silaha Hamas, utawala wa Gaza baada ya vita na muundo na mamlaka ya kikosi cha usalama cha kimataifa katika eneo hilo.

“Waziri Mkuu atakutana na Rais Trump siku ya Jumatatu, Desemba 29 watajadili hatua na awamu zijazo na kikosi cha kimataifa cha utulivu wa mpango wa kusitisha mapigano,” msemaji wa serikali Shosh Bedrosian amesema katika mkutano wa mtandaoni na waandishi wa habari.

Mnamo Desemba 1, Ofisi ya waziri mkuu ilisema kwamba Trump amemwalika Netanyahu kwenye Ikulu ya White House. Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kwamba viongozi hao wawili wanaweza kukutana huko Florida.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *