“Kurudi Umoja wa Mataifa ni kama kurudi nyumbani,” amesema mwanasiasa huyo wa Korea Kusini hii leo, akiwa New York, mahali anapopafahamu vyema kiasi cha kutoweza kupuuza nyufa zake. Akihutubia mabalozi, Bw. Ban hakufika kusherehekea historia yake, bali kutoa tathmini nzito: taasisi iliyo dhaifu, inayokabiliwa na migogoro mingi na kuzuiwa na miundo yake ya madaraka.

Alikumbusha kuwa dunia haijatulia tangu aondoke. Badala yake, imekuwa ngumu zaidi. Uvamizi wa Ukraine uliofanywa na mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama, vifo vingi vya raia Gaza, pamoja na kudhoofika kwa ushirikiano wa kimataifa katika muktadha wa mzozo wa tabianchi, kwa mtazamo wake, vimegeuza mgogoro wa kimataifa kuwa “mgogoro wa Umoja wa Mataifa.” Msingi wa tatizo, alisema, ni Baraza la Usalama lenyewe, ambalo “kutoweza kwake kuendelea kufanya kazi ipasavyo” ni “chanzo kikuu cha hali hii.”

Photo

Aliyekuwa Katibu wa Umoja wa Mataifa, RicardoGeneral Ban Kihomoon, alitoa hotuba kwenye mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu amani na usalama wa kimataifa.

UN Photo COEkinder Debebe

Aliyekuwa Katibu wa Umoja wa Mataifa, accordinghGeneral Ban Kihomoon, huhutubia mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu kudumisha amani na usalama wa kimataifa.

Baraza la Usalama likikabiliwa na udhaifu wake

Tathmini yake iko wazi. Mkuu huyo wa zamani wa UN anazishutumu baadhi ya nchi wanachama wa kudumu kwa kulidhoofisha Baraza la Usalama kwa kutumia kura ya turufu kujilinda wao wenyewe, washirika wao au wawakilishi wao. Bila mageuzi, anaonya, “hisia ya kutokuwa na uwezo ndani ya Umoja wa Mataifa haitaondoka. Raia wataendelea kutokulindwa katika migogoro. Kutokuwajibika kutaendelea kutawala.”

Lakini nyuma ya ukosoaji huu wa taasisi kuna swali la kisiasa zaidi: uchaguzi wa Katibu Mkuu ajaye, nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na António Guterres, ambaye muhula wake wa pili unamalizika mwaka 2026.

Kwa Bw. Ban, mchakato wa uteuzi na muda wa muhula vinachangia kudhoofisha nafasi hiyo. Anapendekeza muhula mmoja wa miaka saba, akisema kuwa mihula miwili ya miaka mitano humfanya Katibu Mkuu “kuwa tegemezi kupita kiasi” kwa wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama. Mipangilio hii, anabainisha, haipo katika Mkataba wa kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa na inaweza kurekebishwa na Mkutano Mkuu.

Kwa sababu, anasisitiza Ban Ki-moon, mamlaka ya kimaadili pekee haitoshi. “Lazima pia wawe na nguvu halisi ya kupatanisha pande zinazokinzana na kuingilia kati kwa uwazi zaidi pale kunapokuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa,” hususan mbele ya uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu. Kwa maneno mengine, Katibu Mkuu asiye chini ya shinikizo la kuchaguliwa tena, mwenye uwezo wa kuzungumza kwa niaba ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa, na asiye chini ya kivuli cha kura za turufu.

media:entermedia_image:d30f79a2-8c2f-4562-8936-a9d12419537e

UN Photo/Mark Garten

Makatibu Wakuu wa zamani Kofi Annan (kushoto) na Ban Ki-moon (kulia) wakiwa na Katibu Mkuu António Guterres kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.

Nafasi yenye rasilimali chache, maana kubwa

Mvutano huu kati ya udhaifu wa nyenzo na wajibu wa kimaadili ulikuwa kiini cha mchango wa Anjali Dayal, profesa katika Chuo Kikuu cha Fordham, ambaye pia alialikwa kuzungumza mbele ya Baraza. Kwa mtazamo wake, Katibu Mkuu ajaye atarithi taasisi “yenye uwezo uliopungua sana,” inayokabwa na mgogoro wa kifedha utakaotafsiriwa moja kwa moja kuwa “watoto wachanga wachache kuchanjwa,” “chakula kidogo kwa raia waliokwama katika migogoro,” au “mabomu machache ya ardhini kuondolewa kwenye maeneo ambako watoto hucheza.”

Hata hivyo, anasisitiza, nchi zinaendelea kukutana. Licha ya vikwazo na migawanyiko, “nyote mpo hapa.” Uwepo huo, anasema, unaonesha imani endelevu kuwa ushirikiano wa kimataifa bado ni bora kuliko mantiki ya kila mmoja kivyake. Katika lugha ya mahusiano ya kimataifa, anaeleza, ushirikiano unawezekana pale nchi zinapothamini zaidi mustakabali kuliko faida za haraka.

Hapa ndipo, kwa mujibu wa Anjali Dayal, asili ya uongozi unaotarajiwa ilipo. Katibu Mkuu ana rasilimali chache za kimwili, “fedha kidogo na mamlaka rasmi kidogo.” Lakini anamiliki jambo jingine: “nguvu ya mawazo na simulizi,” “mamlaka ya kipekee ya kimaadili ya dunia nzima” ya kutetea amani na maslahi ya pamoja, pamoja na uwezo wa kuhamasisha mifumo ya Umoja wa Mataifa kuelekea malengo yaliyowekwa na Nchi Wanachama.

Mchakato rasmi na usio rasmi

Uteuzi wa mkuu ajaye wa taasisi ni sehemu ya utaratibu uliowekwa. Mchakato ulizinduliwa rasmi tarehe 25 Novemba 2025 kupitia barua ya pamoja ya Rais wa Mkutano Mkuu na Rais wa Baraza la Usalama, iliyozialika nchi wanachama kuwasilisha majina ya wagombea.

Wagombea, waliopendekezwa na nchi moja au zaidi, wanapaswa kuwasilisha taarifa ya maono yao, wasifu binafsi, na taarifa kuhusu ufadhili wa kampeni kabla ya kushiriki katika mazungumzo ya wazi yanayoandaliwa na Mkutano Mkuu. Orodha ya wagombea huwekwa wazi na kusahihishwa mara kwa mara ili kuhusisha kwa karibu nchi zote wanachama, ingawa pendekezo la mwisho, kwa vitendo, hubaki mikononi mwa Baraza la Usalama.

media:entermedia_image:66d26892-19c9-4933-956d-c5244c5b107a

UN Photo/Loey Felipe

Anjali Dayal, Profesa Mshiriki wa Siasa za Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Fordham, akihutubia Baraza la Usalama.

Kuwekeza katika kesho

Historia, anakumbusha Anjali Dayal, inaonesha kuwa mamlaka hii inaweza kuwa na uzito, hata katika nyakati zenye mgawanyiko mkubwa. Javier Pérez de Cuéllar, aliyechaguliwa baada ya wiki sita za mkwamo wakati wa Vita Baridi, na U Thant, mbunifu wa kimya wa suluhu ya amani ya mgogoro wa makombora ya Cuba, ni mifano dhahiri. Sifa yao ya pamoja: uwezo wa kuangalia zaidi ya maslahi ya haraka na kuweka hatua za kimataifa katika mtazamo wa muda mrefu.

Hili, Anjali Dayal anahitimisha, huenda ndilo “sifa muhimu zaidi” ya Katibu Mkuu ajaye: mtu anayethamini “kesho kuliko faida za leo,” na anayeelewa kuwa dhamira yake ni “ya ubinadamu wote.”

New York, majadiliano yanapoanza kuhusu mrithi wa António Guterres, michango ya Ban Ki-moon na Anjali Dayal inaungana katika onyo moja. Bila mageuzi ya Baraza la Usalama, bila ufafanuzi wa jukumu na uhuru wa Katibu Mkuu, Umoja wa Mataifa uko katika hatari ya kubaki dira ya kimaadili isiyo na ushawishi wa kweli katika dunia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *