Kupitia kampeni hii, baadhi ya wananchi, ikiwemo wanaofanya biashara za kuuza miili yao, madereva, na wahudumu wa afya, walipewa fursa ya kupokea chanjo kupitia mabasi ya kudumu na ya muda, huku uhamasishaji wa kijamii ukihakikisha ujumbe wa kinga unafikika kwa wengi.

Imani Baraka, Mratibu wa chanjo Mombasa, ametoa maelezo kuhusu jinsi dozi za chanjo zilivyopokelewa na mikakati ya kusambaza chanjo kwa wananchi. “Kaunti ya Mombasa imepokea dozi 5,000 za chanjo ya Mpox ambazo zimetolewa kwetu ili kulenga kaunti ndogo mbili ambazo awali zilikuwa zimeshuhudia kuenea kwa mlipuko wa Mpox kwa kiwango kikubwa. Mikakati ya usambazaji wa chanjo ilikuwa kupitia vituo vya kudumu ambapo tulikuwa na vifaa kama vile vituo vya afya vya Port Reitz, Miritini na Mikindani ambapo tulikuwa tunatoa chanjo kwa watu waliolengwa. Pia tulikuwa na vituo vya muda vilivyowekwa ambapo tulihama kutoka sehemu moja hadi nyingine tukilenga maeneo yenye mlipuko mkali.”

Kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Mpox inazidi kuimarika katika Kaunti ya Mombasa, huku wananchi wengi wakichukua hatua za kujilinda kutokana na hatari za virusi hii.

Pamela Atieno, ambaye ni mwalimu wa wenzake , anaeleza sababu za kuchukua chanjo na jinsi mchakato ulivyokuwa katika vituo vya chanjo. “Niliamua kupokea chanjo ya Mpox baada ya kufundishwa kuhusu hatari za virusi. Kwa sababu ya aina ya kazi yangu, ninaweza kwa urahisi kuathirika na virusi hivyo, ndiyo maana niliamua kuchukua chanjo ya MPOX ili kujilinda. Tulielezwa kwamba tukitembelea baadhi ya vituo tunaweza kupata chanjo. Nilienda nikapokea chanjo na nilikuwa nimefafanuliwa kuhusu madhara yanayoweza kutokea kutokana na chanjo hiyo. Kwenye kituo tulipewa fomu za ridhaa (consent forms) tulizosoma, kuelewa masharti, kusaini kisha kupokea chanjo.”

Caroline Agutu, Afisa Uhamasishaji wa Afya wa Kaunti ya Mombasa anasema UNICEF kupitia ufadhili wa Mastercard Foundation na Latter Day Saints walitusaidia kama kaunti kuhakikisha tunaweza kufikia hadhira tuliyolenga, ikiwemo wafanyakazi wa kike na madereva wa malori, ili waweze kuja kwa wingi kupata chanjo ya Mpox.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *