Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ada mpya ya usalama wa uwanja wa ndege itaanzishwa hivi karibuni. Kiasi: dola 30 kwa kila abiria. Itatumika kwa safari zote za ndege za kimataifa, zinazotoka na kuwasili DRC, kulingana na hati ambazo RFI imepata. Lengo: kufadhili utekelezaji wa mfumo jumuishi wa usalama na uhamiaji.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kulingana na afisa wa serikali aliyewasiliana na RFI, dola 30 itaongezwa kwenye bei ya tikiti kwa safari zote za ndege za kimataifa za kibiashara. Ada hii itakusanywa na mashirika ya ndege. Imekusudiwa kutoa huduma bora za udhibiti wa usalama katika mipaka ya DRC. Kulingana na chanzo hicho, hii ni sehemu ya kifurushi cha kifedha kilichoundwa ili kufunga mfumo mzuri wa usalama, udhibiti wa ufikiaji, na ukusughuliki mamombi ya  uhamiaji.

Mkataba unachukua umbo la ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi. Ulisainiwa na kampuni ya Marekani ya Securiport LLC, ambayo tayari imefanya kazi na nchi zingine za Afrika. Chini ya usambazaji uliopendekezwa, 15% ya mapato yataenda kwa serikali ya DRC na 85% kwa Securiport.

Ada nyingine ya dola 50 tayari ipo

Lakini suala hilo tayari linasababisha kutoridhika nchini DRC. Abiria kwenye ndege za kimataifa tayari wanalipa Go Pass ya dola 50, ada iliyoanzishwa mwaka wa 2009 ambayo imekosolewa vikali.

Go Pass hii ilikusudiwa kufadhili uboreshaji wa miundombinu ya viwanja vya ndege, lakini ukosefu wa uwazi kuhusu matumizi ya fedha hizi ulisababisha Bunge kuomba uchunguzi, na Kinshasa sasa inakubali kwamba baadhi ya vifungu vya mkataba wa Go Pass haviwezi kurekebishwa tena.

Kulingana na RFI, taarifa rasmi ya serikali inatarajiwa kutoa maelezo kamili kuhusu ada mpya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *