Kulingana na Budapest, Rais wa Marekani Donald Trump amekubali siku ya Ijumaa, Novemba 7, kuipa Hungary msamaha wa vikwazo vya Marekani vinavyohusiana na mafuta ya Urusi. Msamaha huo uliripotiwa kutolewa wakati wa mkutano na Waziri Mkuu Viktor Orban, ambaye sera zake za kupinga uhamiaji alizisifu sana.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Matokeo makubwa ya mkutano wa leo [kati ya Rais wa Marekani na kiongozi wa Hungary]: Marekani imeipa Hungary msamaha usio na kikomo wa vikwazo vya mafuta na gesi ya Urusi. Tunashukuru kwa uamuzi huu, ambao unahakikisha usalama wa nishati wa Hungary,” Waziri wa Mambo ya Nje wa Hungary Peter Szijjarto ameandika kwenye mtandao wa kijamii wa X.

Kabla ya mkutano wake na Viktor Orban, Donald Trump alithibitisha kuwa alikuwa akifikiria uwezekano wa msamaha huo, kwa sababu ni “vigumu sana” kwa mshirika wake “kupata mafuta na gesi kutoka maeneo mengine” kwa kuwa Hungary “haina ufikiaji wa bahari.” Waziri Mkuu wa Hungary amekuwa mfuasi wa bilionea huyo wa Marekani tangu kampeni yake ya kwanza akiwania kiti cha rais mnamo mwaka 2016. Alionyesha kwamba alikusudia kumweleza, wakati wa mkutano wao wa pande mbili, “matokeo” kwa Hungary ya “kutokuwa tena na gesi na mafuta ya Urusi.”

Mnamo mwezi Oktoba, Marekani iliweka vikwazo kwa maskampuni mawili makubwa ya uzalishaji wa mafuta ya Urusi – Rosneft na Lukoil – kujibu kukataa kwa Urusi kukomesha vita nchini Ukraine. Washington pia ilizitaka nchi kama Slovakia na Hungary “kujiondoa” kutoka kwa vyanzo vya nishati vya Urusi. Budapest inategemea sana mafuta ya Urusi, na vikwazo vya Marekani vinaweza kumuweka hatarini Viktor Orban, miezi michache tu kabla ya uchaguzi wa bunge ambapo kiongozi huyo aliye madarakani tangu mwaka 2010, hana uhakika wa kushinda, kulingana na uchunguzi wa kura za maoni.

Kwa hivyo, makubaliano haya kutoka kwa Donald Trump, yaliyotangazwa na Hungary Ijumaa, Novemba 7, pamoja na msamaha huu, ni habari njema kwa nchi hii ya Ulaya ya Kati, ingawa, baadaye kidogo, afisa wa Ikulu ya White House alionyesha kwamba yalitolewa kwa Budapest kwa mwaka mmoja tu. Kwa upande mwingine, Hungary imejitolea kununua gesi asilia iliyoyeyushwa ya Marekani kwa dola milioni 600 , chanzo hicho kinasema.

“Ilikuwa mkutano wa kihistoria; Hungary ni mdau muhimu duniani,” televisheni ya umma ya Hungary imesema ikionyesha furaha yake. “Tulifanikiwa!” limeongeza gazeti la kila siku linalounga mkono Orban Magyar Nemzet. Vyombo vya habari vinavyounga mkono serikali vimesifu kwa ushindi ujuzi wa mazungumzo wa Viktor Orban, anaripoti mwandishi wetu huko Budapest, Florence La Bruyère.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *