Waendesha mashtaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC, wanataka kiongozi wa kundi la Janjaweed Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, maarufu kwa jina la Ali Kushayb, ambaye wapiganaji wake walisababisha mauaji makubwa kwenye jimbo la Darfur nchini Sudan, wanataka ahukumiwe maisha jela.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Waendesha mashtaka hao wakiongozwa na Julian Nicholls wameiambia Mahakama, Al-Rahman mwenye umri wa miaka 76, wakati mmoja alitumia shoka kuua watu wawili na kumtaja kama mhusika mkuu na hatari kufuatia misururu wa vitendo vya ukatili dhidi ya watu wasio na hatia , katika eneo la Darfur zaidi ya miaka 20 iliyopita.
Oktoba 7, alipatikana na hatia kwa kutekeleza makosa 27 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, hatua ambayo imeonekana kuwa mafanikio ya kwanza ya mahakama ya mahakama hiyo yanayohusishwa na mzozo huo.

Nao Mawakili wa Al-Rahman wanaapinga mapendekezo hayo ya waendesha mashtaka wakimtaja mshitakiwa kuwa asiye na hatia na wakaahidi kuwasilisha maoni yao juu ya hukumu yake baadaye wiki hii.
Mzozo wa Darfur ulizuka kwa mara ya kwanza mwaka 2003 wakati waasi wengi wasio Waarabu walipochukua silaha dhidi ya serikali ya Sudan, wakiishutumu serkali kutenga eneo la magharibi mwa nchi hiyo.