Ni mwaka mooja leo Alhamisi, Novemba 27, 2025, tangu kusainiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano yalipoanza kutumika kinadharia kati ya Israel na Lebanon. Yalitiwa saini baada ya makabiliano makali kati ya jeshi la Israel na Hezbollah ya Lebanon. Mapigano hayo yalisababisha Hezbollah kudhoofika sana kijeshi na kisiasa, huku kiongozi wake, Hassan Nasrallah, akiuawa katika shambulio la anga la Israel. Hata hivyo, mwaka mmoja baadaye, hali bado ni tete.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Hakutakuwa na utulivu Lebanon hadi usalama wa taifa la Israel utakapohakikishwa.” Haya ni maneno ya Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz, huku Israel ikiendesha mashambulizi ya anga karibu kila siku katika eneo la Lebanon. Mashambulizi yanazidi kuongezeka. Siku ya Jumapili, afisa mkuu wa Hezbollah aliuawa katika shambulio la bomu katika vitongoji vya kusini mwa Beirut.

Kwa hivyo, kusitisha mapigano si kusitisha mapigano kwa Israel, ambayo jeshi lake bado halijajiondoa kutoka ngome kadhaa za mpakani, kinyume na makubaliano ya mwezi Novemba mwaka uliyopita.

Hezbollah imedhoofika

Hezbollah, ikiwa imedhoofika sana, haionekani kuwa na njia za kujibu shinikizo hili linaloendelea, lakini kundi hili la kisiasa na kijeshi bado linakataa kupokonywa silaha kabisa, kwa agizo la serikali ya Lebanon yenyewe. Na mashambulizi ya anga ya Israel yanafanya Hezbollah kusita sita.

Katika muktadha huu, viongozi wa Lebanon wenyewe wanakabiliwa na shinikizo kubwa la kisiasa kutoka Marekani, ambayo katika suala hili inaendana na misimamo ya Israel, iliyoazimia kupunguza zaidi ushawishi wa kikanda wa Iran na washirika wake, ikiwa ni pamoja na Hezbollah ya Lebanon.

Hofu ya kuongezeka kwa uhasama

Siku ya jumatano Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri alisema kwamba nchi yake ilikuwa ikifanya kazi ili kupunguza mvutano kati ya Israel na kundi lenye silaha la Lebanon linaloungwa mkono na Iran. “Tunaogopa ongezeko lolote la mapigano na tuna wasiwasi kuhusu usalama na utulivu wa Lebanon,” alisema waziri huyo, Badr Abdel Ati, baada ya kukutana na Rais wa Lebanon Joseph Aoun huko Beirut siku ya Jumatano. “Tunafanya juhudi kubwa za kuiokoa Lebanon kutokana na hatari au madhara yoyote kwa usalama wake,” ameongeza.

Chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano, jeshi la Lebanon linapaswa kubomoa uwepo wa kijeshi wa Hezbollah katika ukanda wa kilomita 30 (maili 10) kati ya mpaka na Israel na Mto Litani kaskazini zaidi. Jeshi hilo limewasilisha mpango kwa serikali, ambapo linajitolea kukamilisha kazi hii kubwa kabla ya kuendelea hatua kwa hatua hadi eneo nchini kote Lebanon. Lakini Marekani na Israel zinashutumu mamlaka ya Lebanon kwa kuchelewesha hatua dhidi ya upinzani mkali kutoka kwa Hezbollah.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *