Watu 44 wamepoteza maisha jijini Hong Kong huku wengine zaidi ya mia mbili wakiwa hawajulikani walipo,kufuatia mkasa wa moto ulioteketeza jumba lenye orofa 31.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mapema Alhamisi wazima moto bado walikuwa wakipambana kuzima moto huo na shughuli za kuokoa watu katika eneo hilo lenye makazi elfu mbili.

Jumba hilo lilojengwa kwa mti aina ya Bamboo lilishika moto wakati  marekebisho yalipokuwa yakiendelea na madirisha yote yalikuwa yamefungwa hivyo watu wengu hawakufahamu haraka kuwa kuna moto.

Wazima moto wakipambana na moto katika jengo la makazi ya watu huko Hong Kong.
Wazima moto wakipambana na moto katika jengo la makazi ya watu huko Hong Kong. REUTERS – Tyrone Siu

Miongoni mwa watu waliofariki ni mmoja  wa zima moto ambaye alipata majeraha makubwa ya kuungua usoni baada ya kupoteza mawasiliano na wenzake.

Msemaji wa serikali eneo hilo amesema watu 56 wametibiwa hospitalini na kuruhusiwa kuondoka huku wengine 16 wakiwa kwenye hali mahututi.

Mtu aliyejeruhiwa kwa mkasa huo wa moto jijini Hong Kong
Mtu aliyejeruhiwa kwa mkasa huo wa moto jijini Hong Kong REUTERS – Tyrone Siu

Polisi asubuhi hii wamesema wamewakamata watu watatu wanaoshukiwa kuhusika na kisa hicho  baada ya kuacha vifaa vya kushika moto haraka kwenye eneo hilo  wakati wa shughuli za ufundi ,hali inayosemekana kuwa chanzo cha moto huo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *