Saif al-Islam Gaddafi, mtoto wa aliyekuwa Rais wa Libya Muammar Gaddafi, ameripotiwa kuuawa, kulingana na vyanzo vilivyo karibu na familia yake, wakili wake Khaled el-Zaydi, pamoja na vyombo vya habari vya Libya, vilitoa taarifa hiyo siku ya Jumanne.
Hadi sasa hakuna maelezo zaidi kuhusu kifo cha Gaddafi.
Ingawa Saif al-Islam alikuwa maarufu nchini humo, hasa kwa nafasi yake katika kuunda sera za serikali kabla ya mwaka 2011, umaarufu wake hadharani umepungua katika miaka ya hivi karibuni.