Taarifa iliyotolewa hii leo huko jijini Geneva, Uswisi inasema ripoti hiyo iliyopatiwa jina Hali ya Tabianchi Duniani 2025, inaweka bayana kuwa mabadiliko haya ya haraka na makubwa yametokea ndani ya miongo michache, lakini yatakuwa na athari mbaya kwa mamia hata maelfu ya miaka ijayo.

Ujumbe muhimu kutoka kwenye ripoti

  • Miaka 2015–2025 ndiyo miaka 11 yenye joto zaidi kuwahi kurekodiwa duniani.
  • Ukosefu wa uwiano wa nishati ya dunia umefikia kiwango cha juu zaidi katika rekodi ya miaka 6
  • Bahari imekuwa ikifyonza hewa ya ukaa sawa na mara 18 ya matumizi ya nishati ya binadamu kila mwaka katika miongo miwili iliyopita
  • Hali mbaya za hewa kupindukia huwa na madhara kwa mamilioni ya watu na kugharimu mabilioni ya fedha.
  • Maudhui ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani: Chunguza leo ili kulinda kesho.

Thibitisho la viwango vya joto

Ripoti hiyo ya WMO inathibitisha kuwa miaka 2015–2025 ndiyo miaka 11 yenye joto zaidi kuwahi kurekodiwa, na kwamba mwaka 2025 ulikuwa wa pili au wa tatu kwa joto zaidi, ukiwa takribani nyuzi joto 1.43 katika kipimo cha Selsiyasi juu ya wastani wa miaka 1850–1900. Matukio makali duniani kote, yakiwemo joto kali, mvua kubwa na vimbunga vya kitropiki, yalisababisha usumbufu na uharibifu mkubwa na kuonyesha udhaifu wa uchumi na jamii zetu zilizounganishwa.

Kuongeza kasi ya kuyeyuka kwa barafu kunahatarisha kusababisha maporomoko ya athari kwa uchumi, mifumo ikolojia na jamii.

Kuongeza kasi ya kuyeyuka kwa barafu kunahatarisha kusababisha maporomoko ya athari kwa uchumi, mifumo ikolojia na jamii.

Barafu baharini kuyeyuka

Bahari inaendelea kupata joto na kufyonza hewa ya ukaa. Eneo la barafu baharini katika Aktiki lilikuwa katika kiwango cha chini cha kihistoria au karibu na hicho, huku Antaktika ikiwa ya tatu kwa kiwango cha chini kabisa kuwahi kurekodiwa, na kuyeyuka kwa barafu za milimani kuliendelea bila kupungua.

“Hali ya hewa ya dunia iko katika hali ya dharura. Sayari dunia inasukumwa kupita mipaka yake. Kila kiashiria muhimu cha hali ya hewa kinaonesha hatari,” amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kwenye taarifa iliyotolewa kuhusu ripoti hiyo.

“Binadamu wamepitia miaka 11 yenye joto zaidi kuwahi kurekodiwa. Historia inapojirudia mara 11, si jambo la ghafla tena—ni wito wa kuchukua hatua,” amesema Guterres.

Mizani ya nishati iingiayo na itokayo duniani

Kwa mara ya kwanza, ripoti hii inajumuisha ukosefu wa uwiano wa nishati ya dunia kama kiashiria muhimu cha tabianchi.

Uwiano wa nishati ya dunia hupima kasi ambayo nishati inaingia na kutoka katika mfumo wa dunia. Katika hali ya kawaida, nishati inayoingia ya jua hulingana takribani na nishati inayotoka.

Hata hivyo, ongezeko la gesi chafuzi zinazozuia joto—hewa ya ukaa, methani na naitrojeni—limevuruga uwiano huu, zikifikia viwango vya juu zaidi katika angalau miaka 800,000.

Ukosefu wa uwiano wa nishati ya dunia umeongezeka tangu rekodi zilipoanza mwaka 1960, hasa katika miaka 20 iliyopita, na kufikia kiwango kipya cha juu mwaka 2025.

Mwanamume akimsaidia mwanamke baada ya gari lake kukwama kwenye maji yanayofika kiunoni. Mvua duniani inazidi kuwa baya zaidi kutokana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

© WMO/Teguh Prihatna

Mwanamume akimsaidia mwanamke baada ya gari lake kunasa kwenye maji yanayofika kiunoni. Mvua duniani zinazidi kipimo na hii ni kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Kauli ya Guterres

“Maendeleo ya kisayansi yameongeza uelewa wetu wa hali halisi ya sayari yetu na hali ya hewa yake. Shughuli za binadamu zinaendelea kuvuruga uwiano wa asili, na tutaishi na athari hizi kwa mamia na maelfu ya miaka,” amesema Katibu Mkuu wa WMO Celeste Saulo.

“Kila siku, hali ya hewa imekuwa kali zaidi. Mwaka 2025, mawimbi ya joto, moto wa misitu, ukame, vimbunga, dhoruba na mafuriko yalisababisha vifo vya maelfu, kuathiri mamilioni ya watu na kusababisha hasara ya mabilioni ya dola,” ameongeza.

Ongezeko la joto katika anga la juu (hasa karibu na uso wa dunia) linawakilisha takribani asilimia 1 ya nishati ya ziada, huku karibu asilimia 5 ikihifadhiwa kwenye ardhi.

Zaidi ya asilimia 91ya joto hili la ziada huhifadhiwa katika bahari, ambayo hufanya kama kinga dhidi ya ongezeko la joto ardhini. Joto la bahari lilifikia kiwango cha juu zaidi mwaka 2025, na kasi ya ongezeko lake imeongezeka zaidi ya mara mbili kati ya 1960–2005 na 2005–2025.

Takribani asilimia 3 ya nishati ya ziada hutumika kuyeyusha barafu. Barafu katika Antaktika na Greenland kwa kiasi kikubwa zimepotea , na kiwango cha barafu baharini katika Aktiki mwaka 2025 kilikuwa cha chini kabisa au cha pili kwa chini tangu vipimo vya satelaiti vianze. Upotevu mkubwa wa barafu ulitokea Iceland na pwani ya Pasifiki ya Amerika Kaskazini.

Kwa mujibu wa wataalamu, hali hii itaendelea kwa karne nyingi, na baadhi ya mabadiliko haya hayawezi kurekebishwa kwa maelfu ya miaka.

media:entermedia_image:77a58e78-4c6a-4356-ad4b-1ce0ef46e615

© WMO/Arya Manggala

Kila mwaka hali mbaya ya hewa ya kupindukia pamoja na mabadiliko ya tabianchi yanakuwa na madhara makubwa sio tu kwa uchumi duniani bali pia kwa binadamu.

Madhara yake kwa binadamu 

Ripoti hii pia inaonesha athari za matukio makali, ikiwemo uhaba wa chakula na kuhama kwa watu, pamoja na athari mbayá za hali ya hewa kwa afya kama vile kuenea kwa magonjwa kama dengue na msongo anaopata binadamu kutokana na joto kali.

“Inaonesha ukweli mwingine: uraibu wetu kwa nishati ya mafuta kisukuku unavuruga tabianchi na usalama wa dunia. Janga la tabianchi linaongezeka, na kuchelewa kuchukua hatua ni hatari,” amesema Guterres.

Soma ripoti nzima hapa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *