
Hatima ya mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifui (ICC), Karim Khan, bado haijulikani. Katika ripoti ya siri iliyowasilishwa kwa nchi wanachama wa ICC mnamo Machi 9, majaji watatu walimsafisha kwa makosa ya utovu wa nidhamu ya kingono dhidi ya mfanyakazi katika ofisi yake.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Hakuna ushahidi wa kutosha kuunga mkono hitimisho la utovu wa nidhamu” wa Karim Khan “mbali na mashaka tu,” majaji watatu huru wa ICC waliandika.
Hitimisho la majaji linatokana na uchunguzi wa Umoja wa Mataifa, anaelezea mwandishi wetu huko Hague, Stéphanie Maupas. Majaji hao watatu wamekosoa vikali ubora wa uchunguzi huu, ambao, kulingana nao, unaonyesha taarifa mbili “zinazopingana kabisa” kuhusu Karim Khan na mlalamikaji, na walishindwa kutoa ushahidi wa hatia ya mwendesha mashtaka.
Kesi hii inaweka dosari kwa ICC kwa karibu miaka miwili. Karim Khan alilazimika kujiuzulu kutoka wadhifa wake mnamo mwezi Mei 2025 wakati uchunguzi ulipokuwa ukiendelea. Huko Hague, nchi wanachama zimegawanyika kuhusu jinsi ya kuendelea na kesi hiyo.
Ripoti hizo mbili sasa ziko mikononi mwa nchi 21 wanachama zinazounda Ofisi ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Nchi hizo zina hadi Aprili 8 kuamua, ikiwezekana kwa makubaliano. Ingawa, kulingana na vyanzo kadhaa, nchi nyingi zinataka kukubali hitimisho la majaji watatu, wengine wanataka kuzuia mwendesha mashtaka kurudi Mahakamani na kuchukua nafasi yake.
Kesi hii inazidisha hali ya ICC, ambayo iko chini ya tishio la vikwazo vipya kutoka kwa utawala wa Trump, wakati Marekani ikitaka kufutwa kwa hati za kukamatwa dhidi ya Benjamin Netanyahu na Waziri wa zamani wa Ulinzi Yoav Gallant, zilizotolewa mwezi Novemba 2024. Shutuma dhidi ya Karim Khan ziliwekwa hadharani wiki chache zilizopita.