Jumla ya Shilingi Bilioni 14 za Kitanzania zimetolewa na serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kutekeleza mradi wa ujenzi wa Daraja la Nzali, Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma na kuondoa adha ya kukatika kwa mawasiliano pamoja na mafuriko kwa wananchi wa Vijiji viwili vya Nzali na Mahama.
Mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huo na kuanza kutumika kwa daraja hilo, wananchi wa Vijiji hivyo pamoja na maeneo mengine ya Chamwino wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa daraja hilo, wakieleza kwamba daraja hilo pia limesisimua uchumi wa wakulima, wafugaji na wafanyabiashara wa Vijiji hivyo na maeneo jirani kutokana na uhakika wa sasa wa usafiri katika misimu yote ya mwaka ndani ya Wilaya hiyo.
#kilichoborakabisa
(Feed generated with FetchRSS)