
Bunge la Israeli limepitisha sheria yenye utata Jumatatu jioni, Machi 30, inayoidhinisha adhabu ya kifo kwa magaidi. Kiutendaji, sheria hii inatarajiwa kutumika tu kwa Wapalestina waliohukumiwa kwa mashambulizi au vitendo vya vurugu dhidi ya Israel.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Kwa msaada wa Mungu, tutawaua maadui zetu”: hivi ndivyo mrengo wa kidini wa kulia ulivyokaribisha kura. Muswada huo ambao ulitetewa na Waziri wa Usalama wa Kitaifa Itamar Ben-Gvir, ulipitishwa kwa usomaji wake wa tatu kwa kura 62 dhidi ya 48 katika bunge la Israel. Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alipiga kura ya kuunga mkono sheria hiyo.
Hasa, sheria hiyo inalenga mauaji yaliyofanywa kwa nia ya “kukataa kuwepo kwa taifa la Israel,” anaripoti mwandishi wetu huko Jerusalem, Michel Paul. Muundo ambao, kulingana na mashirika yasiyo ya kiserikali, unawatenga raia wa Kiyahudi, ukilenga Wapalestina pekee. Mtu aliyehukumiwa atauawa kwa kunyongwa ndani ya siku 90.
Muswada huo pia unaeleza kwamba idadi ndogo ya majaji inatosha kutoa hukumu hiyo na inakataza kuachiliwa kwa mtu yoyote katika kubadilishana wafungwa siku zijazo. Ingawa serikali inazungumzia “kitendo cha haki” na Marekani inatangaza kwamba inaheshimu “haki ya uhuru wa Israel ya kuweka sheria na vikwazo vyake dhidi ya wale wanaopatikana na hatia ya ugaidi,” upinzani na Umoja wa Ulaya wanalaani mkondo wa ubaguzi wa rangi unaodhoofisha utawala wa sheria na kuliweka taifa la Kiyahudi katika ukiukaji wa mikataba ya kimataifa.
Rufaa kwa Mahakama kuu kupinga sheria hiyo
Dakika chache baada ya kupitishwa na Bunge la Israel, Knesset), shirika lisilo la kiserikali la haki za binadamu la Israel lilitangaza kwamba limewasilisha rufaa kwa Mahakama Kuu ya Israel kupinga sheria hiyo. “Ni kinyume na katiba, ni ya kibaguzi kwa asili, na, kwa Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi, na ilipitishwa bila msingi wa kisheria,” kinaandika Chama cha Haki za Kiraia nchini Israel (ACRI) katika taarifa inayoelezea sababu za changamoto yake ya kisheria.
ACRI inataja “hoja mbili huru za kisheria, kila moja inatosha peke yake kuibatilisha sheria.” Kwanza, inasema, Bunge la Israel “halina mamlaka ya kutunga sheria kuhusu Ukingo wa Magharibi,” eneo la Palestina linalokaliwa na Israel tangu mwaka 1967 na ambalo taifa la Kiyahudi “halitumii uhuru wowote.” “Chini ya sheria ya kimataifa inayosimamia uvamizi wa kijeshi, mamlaka ya kutunga sheria ni ya kamanda wa kijeshi—sio Knesset,” shirika lisilo la kiserikali linaongeza.
Zaidi ya hayo, “sheria hiyo ni kinyume na katiba” kwa sababu “inakiuka haki ya kuishi, utu wa binadamu, haki ya mchakato unaofaa, na kanuni ya usawa—haki zote zinazolindwa” na Sheria za Msingi za Israel, ambazo hutumika kama katiba yake, inaongeza ACRI. Kulingana na shirika hilo lisilo la kiserikali, “sheria inaunda njia mbili zinazofanana, zote zimeundwa kutumika kwa Wapalestina pekee.”
Mamlaka ya Palestina ililaani jaribio la “kuhalalisha mauaji yasiyopitishwa na mahakama.” Sheria hii inaunda “uhalifu na ongezeko hatari katika sera za uvamizi [unaotekelezwa na Israel] halina uhuru juu ya ardhi ya Palestina,” inaandika Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina, ambayo sheria hii “inafichua tena asili ya mfumo wa kikoloni wa Israeli,” kwa kutafuta “kuhalalisha mauaji yasiyopitishwa na mahakama kwa kuyapa nafasi ya kisheria.”