Taarifa iliyochapishwa kwenye wavuti wa WHO imeeleza kuwa, wagonjwa wa mwanzo waliripotiwa tarehe 30 Machi 2026, ambapo wengi wao walikuwa ni watu wa familia moja pamoja na wale waliokuwa na mawasiliano ya karibu nao.

Dalili za ugonjwa

Dalili zilizoripotiwa ni pamoja na homa, kutapika, kuharisha, kuwepo kwa damu kwenye mkojo, uchovu na maumivu ya tumbo. Katika baadhi ya wagonjwa wenye hali mbaya zaidi, dalili zimejumuisha pia homa ya manjano na upungufu wa damu.

Vipimo vya awali vya maabara vimebaini kuwa ugonjwa huo siyo Ebola wala Marburg. Hata hivyo, uchunguzi zaidi unaendelea, ukiwemo upimaji wa magonjwa mengine kama vile homa ya Bonde la Ufa, dengue na homa ya manjano.

Timu ya pamoja ya wataalamu kutoka kituo cha kitaifa cha dharura za afya ya umma na maabara ya rufaa ya kitaifa imetumwa eneo la tukio kusaidia uchunguzi wa kina pamoja na kudhibiti mlipuko huo.

WHO Afrika

WHO inaendelea kuisaidia Wizara ya Afya ya Burundi kuimarisha ufuatiliaji wa magonjwa, uchunguzi wa kitabibu, huduma kwa wagonjwa, uchunguzi wa maabara pamoja na hatua za kudhibiti maambukizi.

Aidha, shirika hilo linatoa msaada wa vifaa na uratibu ili kuhakikisha shughuli muhimu zinaendelea bila kukwama.

Waziri wa Afya wa Burundi anaongoza juhudi za kukabiliana na hali hiyo, akishirikiana na wadu wengine ili kuhakikisha mwitikio wa pamoja na wa haraka unatekelezwa kudhibiti ugonjwa huo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *