Iran imekuwa ikifanya tathmini ya gharama ya uharibifu uliosababishwa na vita kama sehemu ya juhudi zake za kujumuisha fidia katika mapendekezo ya kusitisha mapigano, shirika la habari la Tasnim limeripoti.
Akizungumza na vyombo vya habari vya Urusi, msemaji wa serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema makadirio ya awali na ya jumla yanaonyesha kuwa hasara waliopata imefikia takriban dola bilioni 270 kufikia sasa, lakini huenda idadi hiyo ikaongezeka.
Msemaji huyo ameongezea kuwa maafisa wa Iran wanaendelea kufanya tathmini, ambazo zinajumuisha kuangalia uharibifu wa majengo na mapato yaliyopotea kutokana na kusimamishwa kwa shughuli za viwanda na biashara zingine, hii ni kulingana na shirika la habari la Tasnim.
Mohajerani amesema kuwa suala la fidia lilikuwa miongoni mwa mada zilizojadiliwa katika mazungumzo kati ya Marekani na Iran mwishoni mwa wiki iliyopita.

(Feed generated with FetchRSS)