cxv

Chanzo cha picha, Getty Images

Serikali ya Zambia inasema imechukua mwili wa rais wa zamani Edgar Lungu ambaye
alifariki dunia Afrika Kusini miezi 10 iliyopita, uamuzi unaoenda kinyume na
matakwa ya familia yake.

Hili ni tukio la hivi karibuni katika mvutano kuhusu nini kifanyike na
mwili wa kiongozi huyo wa zamani, kufuatia mgogoro wa muda mrefu kati ya Lungu
na mrithi wake, Rais Hakainde Hichilema.

Serikali imesisitiza kuwa, kama aliyewahi kuwa mkuu wa nchi, anapaswa
kupewa heshima ya kitaifa na kuzikwa pamoja na marais wengine waliomtangulia
katika eneo maalum la mazishi ya marais lililopo mji mkuu, Lusaka.

Hata hivyo, familia ya Lungu ilitaka mazishi ya faragha baada ya
mazungumzo na serikali kuhusu mipango ya mazishi kuvunjika.

Mwezi Agosti mwaka jana, mahakama ya Afrika Kusini iliamua kuwa serikali
ya Zambia inaweza kuurudisha mwili huo nyumbani na kufanya mazishi ya kitaifa.

Familia iliwasilisha rufaa kupinga uamuzi huo, lakini kuhamishwa kwa
mwili huo kumefuatia “kutoweza kwao kuendelea na kesi” katika mahakama ya
rufaa, kwa mujibu wa taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Zambia, Mulilo Kabesha.

Akizungumza kwenye kituo cha habari cha YouTube nchini Zambia Jumatano
jioni, msemaji wa familia ya Lungu, Makebi Zulu, alipinga madai kwamba mchakato
wa rufaa ulikuwa umefikia mwisho, akisema taratibu sahihi zilifuatwa.

Sasa mawakili wa familia wamewasilisha ombi la dharura katika mahakama
kuu ya Afrika Kusini ili mwili wa rais huyo wa zamani urejeshwe katika chumba
cha kuhifadhia maiti ambako ulikuwa umehifadhiwa awali.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *