
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeishutumu Marekani leo Jumanne kwa kukiuka makubaliano dhaifu ya usiishaji mapigano kusini mwa nchi, taarifa ambayo inakuja baada ya kutangazwa kwa mashambulizi ya anga ya Marekani.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Jeshi la kigaidi la Marekani, likiendelea na vitendo vyake haramu na visivyo vya haki tangu makubaliano ya kusitisha mapigano (…), lilifanya ukiukaji mkubwa wa makubaliano ya kusitisha mapigano katika eneo la Hormozgan katika kipindi cha saa 48 zilizopita,” wizara hiyo imesema katika taarifa, bila kutaja aina ya tukio hilo.
Kamandi ya jeshi la Marekani Marekani Mashariki ya Kati (Centcom) ilitangaza mapema kwamba ilishambulia maeneo ya kurusha makombora kusini mwa Iran usiku, huku Kikosi cha walinzi wa mapinduzi ya Iran kikisema kimedungua ndege isiyo na rubani ya Marekani na kufyatua risasi kwenye ndege iliyokuwa ikijaribu kuingia anga ya nchi hiyo.
