Iran na Marekani zinadai nini katika mazungumzo yanayoendeleaIran na Marekani zinadai nini katika mazungumzo yanayoendelea

Makubaliano ya awali yanajadiliwa kwa sasa kati ya pande mbalimbali, lakini lengo kuu la Iran ni kupata dhamana ya kudumu ya usalama ili kuondoa kabisa tishio la mgogoro mpya, kwa ajili yake na kwa washirika wake katika eneo hilo. Tehran pia inasisitiza kwamba makubaliano lazima yamalize mgogoro nchini Lebanon.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kwa upande wao, maafisa wa Israel wanabaini kwamba Donald Trump angeunga mkono haki ya Israel ya kuingilia kijeshi popote pale usalama wake unapotishiwa, hasa dhidi ya Hezbollah nchini Lebanon.

Wakati huo huo, Iran inatafuta unafuu kutokana na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa kwenye uchumi wake, hasa kwa kurejesha mali zilizozuiwa katika benki za kigeni. Kwa lengo hili, Tehran inatumia udhibiti wake wa Mlango-Bahari wa Hormuz, njia ya meli ambayo Marekani inataka kurejesha uhuru wa urambazaji.

Kipaumbele kingine kwa Washington ni kuvujwa kwa mpango wa nyuklia wa Iran, kipaumbele cha diplomasia ya Marekani tangu muhula wa kwanza wa Donald Trump. Rais wa Marekani alibainisha kwamba majadiliano hayo yalilenga hasa hatima ya akiba ya uranium iliyorutubishwa ya Iran, ambayo, kulingana naye, inapaswa “kukabidhiwa mara moja kwa Marekani na kuharibiwa, papo hapo au katika eneo lingine linalokubalika.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *