Oburu Oginga amtambulisha kimahaba mkewe wa 2 katika hafla ya maombi ya Kitaifa: “My prayer Warrior”Oburu Oginga amtambulisha kimahaba mkewe wa 2 katika hafla ya maombi ya Kitaifa: “My prayer Warrior”
  • Oburu Oginga alivutia wengi katika hafla ya umma baada ya kuzungumza kwa upendo kuhusu mke wake wa pili Judith na kufichua maelezo ya binafsi yaliyozua hisia mtandaoni
  • “Kinara wa vijana” huyo mwenye umri wa miaka 82 alimiminia Judith sifa tele, akieleza sababu zilizomfanya kuoa mke wa pili, jambo lililowafanya wageni kucheka na kushangilia
  • Judith, anayefanya kazi katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), alieleza furaha na shukrani zake wakati wa utambulisho wa kutoka moyoni uliofanywa na mumewe

Seneta wa Siaya na kiongozi wa ODM, Oburu Oginga, amewavutia Wakenya baada ya kumiminia sifa mke wake wa pili, Judith.

Oburu Oginga na mkewe wa pili katika Ikulu ya Nairobi, wakati wa hafla ya 23 ya Maombi ya Kitaifa.
Mke wa pili wa Oburu Oginga ambaye ni mlokole alivalia suti ya kijani kwenye hafla ya kuombea taifa. Picha: William Ruto.
Source: Facebook

Wakati wa Kiamsha Kinywa cha Kitaifa cha Maombi, kilichokuwa na kaulimbiu ya msamaha na maridhiano, kilichofanyika Alhamisi, Mei 28 katika Ikulu ya Nairobi, viongozi mbalimbali wakiwemo Rais William Ruto, Mama wa Taifa Rachel Ruto, Naibu Rais Kithure Kindiki, Mama wa Taifa Msaidizi Joyce Kindiki, na Oginga Oburu, kutaja wachache tu, walihudhuria.

Pia soma

Mkewe Rais Rachel Ruto awarai Wakenya kuomba na kufunga miezi ya Juni na Julai

Oburu Oginga ana wake wangapi?

Mnamo Oktoba 19, 2025 wakati wa mazishi ya Raila Odinga, Oburu aliwatambulisha kwa upendo wake zake wawili, Dkt Anne na Judith Oburu.

“Kinara huyo wa vijana” alipokuwa akimtambulisha Judith, anayefanya kazi katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), alieleza sababu zilizomfanya kuoa mke wa pili.

Oburu na mkewe wa pili wakipiga picha na wageni nyumbani kwao Nairobi.
Oburu Oginga alifichua kuwa alioa mke wa pili mwenye umri mchanga kwa sababu alitaka mtu wa kumtunza katika uzee wake. Picha: Karungo wa Thang’wa.
Source: Facebook

Muumini huyo wa Kanisa la Anglikana alimiminia mke wake wa pili mapenzi wakati wa hafla ya Kiamsha Kinywa cha Kitaifa cha Maombi, akimsifu kwa kuwa shujaa wa maombi katika familia.

“Niko hapa na mke wangu mpendwa. Watu wengine hawataki kukubali hadharani kwamba wana wake wa pili. Nina mke wa pili ambaye ananitunza. Ameokoka na ni mtu anayesali kwa ajili ya familia yetu. Mimi bado sijafika hapo, lakini ananisukuma nimkaribie zaidi Mungu,” alisema huku akimwalika mke wake kuungana naye jukwaani na kuiombea taifa.

Akiwa amevaa suti ya kijani ya sketi, Judith alikuwa akitabasamu muda wote alipoungana na mume wake mwenye wake wengi jukwaani.

Pia soma

Onyonka asimulia jinsi alivyokutana na Roselyn Akombe akamtosea ndoano ya uchumba: “Mwanamke mjanja”

Aking’aa kwa fahari, Judith alimshukuru mume wake mwenye umri wa miaka 82 kwa kusema maneno mazuri kumhusu.

“Nimeokoka, na ninampenda Bwana kama mwokozi wangu binafsi, na ninafuraha kuwa hapa,” Judith alisema kabla ya kuomba.

Hapa chini ni video:

Subscribe to watch new videos

Wakijibu video hiyo, wanamtandao walivutiwa na mtindo wa Oburu wa ndoa ya wake wengi, huku baadhi wakijiuliza kwa nini mara chache huonekana hadharani akiwa na mke wake wa kwanza.

Maoni yalijumuisha:

Lornah Shibikhwa: “Ndoa zote za wake wengi, wake wa pili huwa wameolewa na mke wa kwanza hubaki kama hajaoa lakini bado haruhusiwi kutoka na mwanaume mwingine huku akiwatunza watoto wake. Msongo wa mawazo huwaangamiza.”

Diana Achieng alisema: “Oburu ni mwanaume wa kimapenzi sana. Anampenda sana mke wake wa pili.”

Jacklin Awuor alisema: “Mapenzi yanaishi hapa.”

Dennis Mwangi aliuliza: “Kwa nini haendi hadharani pamoja na mke wa kwanza, Dkt Anne?”

Naomi Nekesa alisema: “Akiwa na miaka 82 Oburu bado ni wa kimapenzi ilhali mwenzi wangu hawezi hata kunionyesha kwa familia yake au marafiki zake!”

William Ruto alisema nini katika Kiamsha Kinywa cha Kitaifa cha Maombi?

Pia soma

Magazeti ya Kenya, Mei 26: Mwanamume aliyemparamia Ruto huko Kilifi aswekwa ndani kusubiri kesi

Katika taarifa nyingine, William Ruto alisema atakubali matokeo yoyote yatakayojitokeza kutoka kwa Uchaguzi Mkuu wa 2027 wakati wa hafla hiyo ya maombi.

Ruto aliwasihi Wakenya kuacha kuwa na wasiwasi kuhusu uchaguzi wa 2027, akisema nchi inapaswa kuamini mpango wa Mungu kuhusu uongozi.

Ruto pia alizungumzia viwango vya vifo vya kina mama na watoto nchini, akisema Kenya haipaswi kupoteza maisha zaidi kutokana na sababu zinazoweza kuzuilika.

Kiongozi huyo wa taifa, ambaye alifunga ndoa mwaka 1991, alifichua kwa mara ya kwanza kwamba yeye na Rachel walimpoteza mtoto wao wa kwanza wa kiume.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *