
Dk. Mark Godeschalk – au “Dk. Mark” – ni daktari mmisionari kutoka Uholanzi. Amekuwa DRC tangu mwaka 2018 na anafanya kazi kwa jumuiya ya Emmanuel CE39, kanisa la Kiprotestanti katika eneo la Ituri. Akiwa ameishinhuko Nyankunde, kisha Lolwa, na hatimaye Bunia tangu mwaka 2022, husafiri kila mara kusimamia vituo vya afya zaidi ya 40.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Wiki mbili zilizopita, “Dk. Mark” alizungumza na muuguzi mkuu katika kituo cha afya cha Abelkozo, kilomita 15 kutoka Mongbwalu. Muuguzi alimwambia, “Nina wagonjwa watatu au wanne hapa. Hakika ni ugonjwa wa virusi vya Ebola. Lakini kwa bahati mbaya, nimeweza tu kuwaweka karantini. Hakuna usafiri. Hatuwezi kuwapeleka kituo cha matibabu. Wanakaa hapa.” Baadhi wamefariki wakiwa hapa. Muuguzi anakosa vifaa muhimu vya kuwatibu. Pia anakosa vifaa vya kujikinga.
“Huu sio mfano pekee,” anasema “Dk. Mark.” “Kuna vituo kadhaa ambapo unakuta tatizo ni kama hilo.”
Tatizo pia ni la vifaa. Kwa kawaida, kila mgonjwa anayeshukiwa anapaswa kupimwa na kuwekwa karantini. Lakini baadhi ya vituo vya afya vijijini nchini DRC havina vyumba vya kuweka karantini waginjwa wanoshukiwa ugonjwa huo. Kwa hivyo, wagonjwa wanapaswa kusafirishwa hadi vituo vinavyoweza kuwahudumia. Hata hivyo, magari ya wagonjwa ni machache. Mwanzoni mwa mlipuko huo, madereva wa teksi na waendesha pikipiki wakati mwingine walitimiza jukumu hili. Baadhi walisimama. Walielewa hatari. “Usafiri ukawa mgumu,” anasema daktari huyu aliyetoka Uholanzi.
Muuguzi aliyezikwa karibu na kituo chake
Wiki iliyopita, “Dk. Mark” alikuwa katika kijiji kilicho umbali wa kilomita 15 kutoka Mongbwalu. Muuguzi hapo alikuwa mgonjwa wiki kadhaa zilizopita. Alifariki. Alizikwa hapo, karibu na kituo cha afya ambapo alifanya kazi. “Nilikuwepo. Ni hali ya kusikitisha kweli,” daktari anasema.
Anachokiona wakati wa safari zake ni ukosefu wa usawa: “Labda umakini mwingi unaelekezwa katika maeneo yenye hospitali kubwa, labda umakini mwingi katika maeneo yenye miji au vituo. Lakini katikati, kuna vituo vya afya vinavyopokea wagonjwa kwanza.” Na hapo hakuna msaada kupitia majibu kukabiliana na virusi vya Ebola.
“Tulitibu bila kujua ugonjwa”
Mlipuko huo ulitangazwa rasmi Mei 15, 2026. Lakini kulingana na kile wafanyakazi wa afya walimwambia “Dk. Mark,” visa vilikuwepo mapema mwezi Machi, labda hatamwezi Februari. Anafafanua mara moja: “Hili ni jambo ambalo sijafanya uchunguzi mwenyewe. Ni kulingana na kauli zao, kutokana na kile wanachoniambia.”
Ilikuwa katika kipindi hiki, kabla ya utambuzi kufanywa, ambapo wafanyakazi wa afya walikuwa katika hatari kubwa. Walikuwa wakiwatibu wagonjwa bila kujua walikuwa wakitibu nini. Hatua za kinga hazikuwa zimewekwa: “Tulikuwa tunaona visa, lakini hatukujua ni ugonjwa gani.”