Wizara ya Fedha imependekeza kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa vifaa vya umeme vinavyotumika kwenye magari. Hatua hii inalenga kupunguza gharama za upatikanaji wa vifaa hivyo na kuongeza matumizi yake nchini.

Aidha, msamaha huo unapendekezwa pia kwa vipuri vya mifumo ya gesi vinavyotumika kwenye magari. Lengo ni kutoa unafuu kwa watumiaji, kupunguza gharama za matengenezo na matumizi ya magari yanayotumia gesi, pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala hapa nchini.

#AzamTVUpdates
Mhariri | John Mbalamwezi

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *