Milio mikubwa ya risasi imesikika tangu alfajiri ya Juni 18, 2026, karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Diori Hamani huko Niamey. Milio ya risasi inaendelea. Eneo hilo limezingirwa. Washambuliaji wamefanikiwa kuingia katika eneo la uwanja wa ndege. Vikosi vya ulinzi na usalama vya Niger viko macho.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Milio mikubwa ya risasi na milipuko imesikika kwa zaidi ya saa moja leo Alhamisi katika uwanja wa ndege huko Niamey, mji mkuu wa Niger, mwandishi wa habari wa shirika la habari la REUTERS ameripoti.

Eneo hilo limezingirwa na vikosi vya usalama, mwandishi wa habari na wakazi wa eneo hilo wameongeza.

Milipuko ya kwanza iliripotiwa yapata saa 12:00 asubuhi (1:00 zaa za Afrika ya Kati), na milio ya risasi ya hapa na pale bado inaendelea kusikika, mwandishi wa habari wa REUTERS anasema.

Chanzo cha usalama kinasema inaonekana kwamba uwanja wa ndege wa Niamey ndio uliolengwa.

Mamlaka ya Niger haijazungumza chochote, kwani nchi hiyo, kama majirani zake wengi, inapambana na uasi unaochochewa na wanajihadi.

Mwezi Januari mwaka huu, kundi lenye silaha linalohusishwa na Al Qaeda lilidai kuhusika na shambulio kwenye uwanja wa ndege wa Niamey.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *