
Baraza Kuu la Maaskofu Katoliki nchini DRC (CENCO) unaandaa mkutano usiookuwa wa kawaida wa siku tatu kuhusu suala la Katiba. Kikao hiki cha mazungumzo kinafanyika kuanzia Juni 18 hadi 20, 2026. Lengo la Kanisa Katoliki ni kupata msimamo wa pamoja. Siku ya Alhamisi, siku ya kwanza mkutano huu, wanachama wa CENCO walisikia hoja kutoka pande zote mbili.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi
“Kikao hiki cha mazungumzo kisichokuwa cha kawaida kiliitishwa kufuatia mvutano unaoongezeka nchini, unaotokana na kampeni ya wengi madarakani kuunga mkono mabadiliko ya katiba,” alitangaza Askofu Donatien Nshole mnamo Juni 18, wakati wa ufunguzi wa mijadala. Changamoto kwa Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Maaskofu Katoliki nchini DRC (CENCO) ni kuwaruhusu maaskofu kuwaruhusu msimamo.
Kisha walimsikiliza Delly Sesanga. Kiongozi wa upinzani, kiongozi wa chama cha Envol, ni mmoja wa kambi hiyo inayopinga vikali mabadiliko yoyote ya katiba. Yeye mwenyewe alijeruhiwa mnamo Juni 12 wakati wa maandamano yalikandamizwa kwa nguvu huko Kinshasa. Alieleza kwamba alitaka kutetea Katiba ya sasa, ambayo inalinda raia dhidi ya uonevu na kuwaruhusu kuchagua viongozi wao kwa uhuru.
Viongozi wa kidini tayari wamegawanyika
Kisha ikawa zamu ya Jean-Claude Tshilumbayi kusikilizwa. Kwa sasa ni Naibu Spika wa Bunge la taifa na mjumbe wa chama cha UDPS cha Rais Félix Tshisekedi. Anaunga mkono mabadiliko ya katiba yanayopendekezwa na serikali. Alirejelea sababu mbalimbali zilizotolewa kutetea marekebisho haya, akikumbusha haswa kwamba ni ahadi ya muda mrefu ya chama, ambacho, mnamo mwaka 2006, kilipinga katiba ya sasa.
Wataalamu na wasomi wa katiba lazima pia wachangie katika mjadala huu, ambao “hautakuwa rahisi,” anaonya mtaalamuwa masuala ya siasa Christian Moleka. Anataja mgawanyiko ndani ya viongozi kidini, kati ya wale wanaopinga mabadiliko yoyote na wale wanaotaka kubaki katika nafasi ya mpatanishi.
“Kati ya maaskofu wanaoamini msimamo thabiti ni muhimu na wale wanaoamini uwezekano wa mazungumzo unapaswa kubaki wazi, mielekeo miwili inayopingana pia inakuwepo ndani ya Kanisa” , anasema Christian Moleka, mtaalamu wa masuala ya siasa na mratibu wa chama cha wataalamu wa masuala ya siasa nchini DRC
Bunge la Kongo lilipitisha muswada mnamo Juni 15, 2026, unaoweka masharti ya kufanyika kwa kura ya maoni nchini DRC, wakati wa kikao cha mwisho cha mkutano wa kawaida wa Bunge, ambao unafanyika tangu mwezi Machi hadi Juni. Rasimu, iliyopitishwa na Bunge la taifa na Baraza la Seneti kwa masharti sawa, itatumwa katika siku zijazo, kwa ajili ya kupitishwa na mkuu wa nchi, ambaye anashutumiwa na upinzani kwa kutaka kuitumia ili kugombea katika uchaguzi wa urais kwa muhula wa tatu.